Namna Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
Namna ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Siku ya Posho ya Kwanza ya Mwezi
“Tunatembelea watu kwa muda mufupi ili kuzungumuza nao kuhusu ulizo hili lenye kushangaza.” [Muonyeshe ulizo la kwanza kwenye ukurasa wa mwisho wa Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 6.] “Wewe unawaza nini?” Acha mutu ajibu. Muzungumuzie habari iliyo chini ya ulizo la kwanza na hata andiko moja. Umutolee magazeti, na upange kumurudilia ili kuzungumuzia ulizo linalofuata.
Munara wa Mulinzi 01/06/14
“Karibu watu 6000000 wanakufa kila mwaka kwa sababu ya kuvuta tumbako. Unawaza ni jambo gani linaweza kufanywa ili kupunguza tatizo hilo? [Acha mutu ajibu.] Watu wengi wamesaidiwa kuacha ao kuepuka kabisa kuvuta tumbako walipojua maoni ya Mungu kuhusu jambo hilo. Kwa mufano, andiko hili la Biblia limewachochea watu fulani wafikirie matokeo mabaya ya kuvuta tumbako juu ya watu wengine. [Soma 1 Wakorintho 10:24.] Gazeti hili linaeleza namna gani kujua maoni ya Mungu kuhusu kuvuta tumbako kunaweza kumuchochea mutu aache kuvuta.”
Amuka! Mwezi wa 6
“Leo, kuliko wakati mwengine wowote, kuzungumuza na watu wengi kwenye Internete kumewawezesha watu wapate wale ambao wanawaza kuwa ni marafiki. Wewe unawaza rafiki wa kweli anapashwa kuwa na sifa gani ya maana? [Acha mutu ajibu.] Ona shauri moja la maana ambalo Biblia inatoa kuhusu rafiki. [Soma Yakobo 1:19.] Gazeti hili linazungumuzia kanuni ine zinazoweza kutusaidia tuwe marafiki wazuri.”