Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 15/05/07
“Namna gani unaweza kujibu ulizo hili? [Soma ulizo kwenye ukurasa wa kwanza. Kisha acha mtu ajibu.] Biblia inatuonyesha kwa nini tunapaswa kuwa na tumaini. [Soma Mathayo 6:9, 10.] Gazeti hili linazungumzia jinsi Ufalme wa Mungu utakavyotimiza mapenzi ya Mungu duniani.”
Amkeni! Mwezi wa 5
“Je, unafikiri kwamba matendo yetu na jambo litakalompata kila mmoja wetu mwishowe vimepangwa na Mungu mbele ya wakati? [Acha mtu ajibu.] Kulingana na andiko hili la Biblia, Mungu anaachia watu uhuru wa kuchagua namna wataishi maisha yao. [Soma Kumbukumbu la Torati 30:19.] Habari hii inaonyesha yale ambayo Biblia inasema kuhusu jambo hilo.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 12.
Mnara wa Mlinzi 01/06/07
“Karibu kila siku tunasikia habari za watu wanaofanya matendo maovu. [Taja mfano moja wa jambo lililotukia sasa linalojulikana kwenu.] Je, umekwisha kujiuliza ikiwa kuna mtu fulani mwovu asiyeonekana anayechochea watu? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Ufunuo 12:12.] Gazeti hili linazungumzia jinsi tunavyoweza kujilinda.”
Amkeni! Mwezi wa 6
“Ningependa nijue mawazo yako kuhusu jambo linalosemwa katika andiko hili. [Soma 1 Timotheo 6:10.] Je, unafikiri kwamba wale wanaofuatia sana feza na vitu vya kimwili wanakuwa na matokeo mabaya mwishowe ? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia matokeo mabaya ya kufuatilia mali.”