Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 01/05/09
Soma Mathayo 24:3. Kisha sema hivi: “Watu fulani wanafikiri kwamba ulizo hili linahusu mwisho wa dunia yetu. Je, unafikiri kwamba dunia itaharibiwa? [Acha mutu ajibu.] Jibu la Yesu linatuonyesha jambo fulani la kutazamia—si mwisho wa dunia, lakini ni mwisho wa kitu kingine. Habari iliyo kwenye ukurasa wa 16 inazungumzia zaidi jambo hilo.”
Amkeni! Mwezi wa 5
“Wahubiri fulani wanasema kwamba ikiwa tunampendeza Mungu, atatupatia utajiri wa kimwili. Lakini, labda unajua watu wema ambao ni maskini. Je, unafikiri kwamba Mungu anataka tuwe matajiri? [Acha mutu ajibu. Kisha soma Waebrania 13:5.] Habari hii inaeleza jinsi Mungu anavyotubariki.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 12.
Mnara wa Mlinzi 01/06/09
“Vitabu vyenye kutoa mashauri yenye kusaidia kuhusu kulea watoto, upendo, na kuhusu jinsi ya kutosheka vinasomwa na watu wengi leo. Je, wewe umeona kwamba vitabu hivyo vinasaidia kweli? [Acha mutu ajibu.] Watu wengi wanapuuza kitabu hiki chenye kutoa mashauri yenye kutegemeka. [Soma 2 Timotheo 3:16.] Gazeti hili linaeleza kwa nini tunaweza kutegemea Biblia na linatoa mashauri fulani yenye kufaa yaliyo katika Biblia.”
Amkeni! Mwezi wa 6
“Kama unavyojua, watu wanabishana sana ikiwa ni vibaya kutoa mimba ao hapana. Je, unafikiri kwamba Biblia inaweza kusaidia mutu anayejiuliza jambo la kufanya katika hali hiyo? [Acha mutu ajibu. Kisha soma 2 Timotheo 3:16, 17.] Gazeti hili linaonyesha yale ambayo Biblia inasema kuhusu kutoa mimba.”