Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 01/05/08
“Kwa kuwa misiba ya asili inaongezeka wakati wetu, watu wengi wanajiuliza ikiwa ni malipizi kutoka kwa Mungu. Unawaza nini? [Acha mtu ajibu. Kisha soma 1 Yohana 4:8.] Habari hii inaonyesha kwa nini Mungu si chanzo cha mateso yanayosababishwa na misiba ya asili.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 30.
Amkeni! Mwezi wa 5
Soma Mathayo 6:10. Kisha uliza: “Je, umekwisha kujiuliza mapenzi ya Mungu ni nini kwa dunia? [Acha matu ajibu.] Kulingana na Biblia, mwanzoni Mungu alikuwa na kusudi kwa dunia, na kusudi hilo halijabadilika. Habari hii inazungumzia jambo hilo.” Kazia habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 10.
Mnara wa Mlinzi 01/06/08
“Moja kati ya hadisi za Biblia zinazojulikana sana ni ile ya Garika ya wakati wa Noa. Je, unafikiri kwamba Garika ilikuwapo kabisa? [Acha mtu ajibu.] Jambo lenye kupendeza ni kwamba, Yesu alizungumzia Garika kuwa jambo lililotukia. [Soma Luka 17:26, 27.] Gazeti hii inatoa sababu za kuamini kwamba Garika ilitukia, na inaonyesha mambo ya maana tunayoweza kujifunza kutokana na Garika.”
Amkeni! Mwezi wa 6
“Ni vigumu kulea watoto, zaidi sana wakati mtoto anakuwa kijana na wakati mwili wake unafanya mabadiliko makubwa. Unafikiri wazazi wanaweza kupata wapi mashauri yenye kutumainika? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Isaya 48:17, 18.] Gazeti hili linatoa mapendekezo ya sasa ili kusaidia wazazi kutenda kwa hekima na uelewevu.”