Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo
Sehemu 3: Matumizi Yenye Matokeo ya Maandiko
1 Tunapoongoza mafunzo ya Biblia mradi wetu ni “kufanya wanafunzi” kwa kusaidia watu waelewe na kukubali mafundisho ya Neno la Mungu na kuyatumia katika maisha zao. (Mt. 28:19, 20; 1 The. 2:13) Kwa hiyo, funzo linapaswa kutegemea Maandiko. Kwanza, litakuwa jambo lenye kusaidia kuonyesha wanafunzi jinsi ya kupata maandiko kamili katika Biblia yao wenyewe. Kwa hiyo, jinsi gani tunavyoweza kutumia Maandiko ili kuwasaidia waendelee kiroho?
2 Chagua Maandiko ya Kusoma: Katika kujitayarisha kwako, tambua jinsi kila andiko ambalo linatajwa katika somo linavyohusiana na habari inayochunguzwa, na uamue ni maandiko gani mtakayosoma na kuzungumzia muda wa funzo lenu. Kwa kawaida, ni vizuri kusoma maandiko yale yanayoonyesha msingi wa Kimaandiko wa mambo tunayoamini. Maandiko ambayo yanatoa habari za ziada huenda hayahitaji kusomwa. Fikiria mahitaji na hali za kila mwanafunzi.
3 Tumia Maulizo: Badala ya kufafanulia mwanafunzi maandiko ya Biblia, mwombe yeye akufafanulie maandiko hayo. Unaweza kumchochea kufanya hivyo kwa kutumia maulizo kwa busara. Ikiwa matumizi ya andiko ni wazi, unaweza tu kuuliza jinsi andiko hilo linaunga mkono yale yanayosemwa katika fungu. Katika visa vingine, ulizo moja kamili au mfululizo wa maulizo yanaweza kuhitajiwa ili kuongoza mwanafunzi kwenye uamuzi unaofaa. Ikiwa maelezo zaidi yanahitajiwa, hayo yanaweza kufanywa baada ya mwanafunzi kujibu.
4 Fanya Habari Iwe Rahisi: Mpiga-mishale mwenye busara anahitaji kwa kawaida mshale moja tu ili kufikia shabaha yake. Hivyohivyo, mwalimu mwenye busara haitaji maneno mengi ili kukazia jambo. Anaweza kufanya habari iwe rahisi, wazi, na sahihi. Wakati mwingine, unaweza kuhitaji kufanya utafiti katika vichapo vya Kikristo ili kuelewa andiko na kulieleza kwa usahihi. (2 Tim. 2:15) Lakini epuka kujaribu kueleza kila sehemu ya kila andiko katika funzo. Tia ndani tu mambo yanayohitajiwa ili kufanya habari mnayojifunza ieleweke.
5 Fanya Matumizi Yanayofaa: Inapofaa, saidia mwanafunzi kuona jinsi maandiko ya Biblia yanavyotumika kwake binafsi. Kwa mfano, mnapochunguza Waebrania 10:24, 25 pamoja na mwanafunzi ambaye hajaanza kuhudhuria mikutano ya Kikristo, unaweza kuzungumzia moja ya mikutano na kumwalika audhurie. Lakini epuka kumkaza. Acha Neno la Mungu limchochee kuchukua uamuzi unaohitajiwa ili kumfurahisha Yehova.—Ebr. 4:12.
6 Tunavyoendelea kutimiza utume wetu wa kufanya wanafunzi, na ‘tuendeleze utii kwa njia ya imani’ kwa kufanya matumizi yenye matokeo ya Maandiko.—Rom. 16:26.
[Maulizo ya Funzo]
1. Kwa nini tunapaswa kukazia Maandiko tunapoongoza mafunzo ya Biblia?
2. Jinsi gani tunavyoamua ni andiko gani la Biblia la kusoma na kuzungumzia?
3. Ni nini faida ya kutumia maulizo, na jinsi gani tunavyoweza kufanya hivyo?
4. Ni maelezo mangapi yanayohitajiwa ili kueleza maandiko tunayosoma?
5, 6. Tunaweza namna gani kusaidia wanafunzi kutumia Neno la Mungu katika maisha yao, lakini tunapaswa kuepuka nini?