Mtolee Yehova Shukrani kwa Ajili ya Fadhili Zake Zenye Upendo—Kifo cha Kristo Kitaadhimishwa Mnamo Machi 24
1 Mtunga-zaburi alisema: “Watu na wamtolee Yehova shukrani kwa ajili ya fadhili zake zenye upendo na kwa ajili ya kazi zake za ajabu kwa wana wa binadamu.” (Zab. 107:8) Fadhili za Mungu zenye upendo ni zaidi ya hisia za uhuruma alizo nazo kuelekea watu. Jambo hilo linaonekana wazi katika maneno yenye kusifu yaliyoongozwa na roho ya Mungu: “Fadhili zako zenye upendo, Ee Yehova, ziliendelea kunitegemeza.” (Zab. 94:18) Kwa kutoa Mwana wake mzaliwa-pekee kwa ajili yetu, Yehova alionyesha fadhili zenye upendo wenye kutokeza kabisa.—1 Yoh. 4:9, 10.
2 Kwa kuwa ukumbusho wa kifo cha Yesu unakaribia, namna gani tunaweza kushukuru “Mungu wa fadhili zenye upendo”? (Zab. 59:17) Kila mmoja wetu atataka kuchukua wakati wa kutafakari kuhusu siku za mwisho za Yesu duniani. (Zab. 143:5) Litakuwa pia jambo lenye faida kufuata usomaji wa pekee wa Biblia unaopangwa kwa ajili ya Ukumbusho, kama inavyoonyeshwa katika Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2005 na, ikiwezekana, kufanya usomaji wa ziada na utafiti katika sura ya 112-116 ya kitabu Mtu Mkuu Zaidi pamoja na vichapo vingine vyenye kutegemea Biblia. Tafakari juu ya maandiko unayosoma, na uzame kabisa katika maandiko hayo. (1 Tim. 4:15) Kufikiria kwa sala Neno la Mungu hakuimarishi moyo wetu tu bali pia kunaonyesha upendo wetu kwa Yehova.—Mt. 22:37.
3 Chochea Wengine Wamtolee Mungu Shukrani: Mwaka uliopita,watu 16,760,607 walihudhuria Ukumbusho ulimwenguni pote. Katika kijiji kimoja huko Liberia, ndugu waliandika barua kwa mkuu wa jiji, wakimujulisha kuhusu maoni yao ya kuadhimisha Mlo wa Jioni wa Bwana katika jiji lake. Mkuu huyo aliwaruhusu ndugu kutumia uwanja wa mpira wa kijiji kwa ajili ya tukio hilo na kufanya watangaze jambo hilo katika eneo lote, wakialika watu kuhudhuria. Ijapokuwa kulikuwa wahubiri watano tu katika kijiji hicho, hudhurio kwenye Ukumbusho lilikuwa la watu 636!
4 Vivyo hivyo, tunataka kusaidia watu wengi iwezekanavyo waambatane nasi kwenye mwadhimisho wa Ukumbusho. Kwa nini usifanye orodha ya wale ambao unataka kualika? Picha kwenye jalada la mbele na la nyuma la Amkeni! ya Machi 8 na Mnara wa Mlinzi wa Machi 15 inatoa mwaliko wa kuudhuria Ukumbusho. Vikaratasi vya mwaliko vilivyochapichwa kwa ajili ya Ukumbusho vinaweza pia kutumiwa. Andika kwa mashine au andika vizuri kwa mkono wakati na mahali pa Ukumbusho kwenye kikaratasi cha mwaliko, na umwachie kila mtu unayealika. Machi 24 inapokaribia, pita tena ili kukumbusha kila mmoja na kuzungumzia mipango ya mwisho.
5 Namna gani tunaweza kusaidia wanafunzi wa Biblia ambao hawajakuja bado kuhudhuria mikutano ili wafaidike kikamili na tukio hilo? Tumia dakika chache kwenye kila funzo ili kuwasaidia waelewe umaana wa mwadhimisho huo. Unaweza kupata habari bora katika Mnara wa Mlinzi wa Machi 15, 2004, ukurasa wa 3-7, na kitabu Kutoa Sababu ukurasa wa 266-269.
6 Karibisha Wageni: Kwenye Ukumbusho, zungumza na wageni na uwakaribishe. (Rom. 12:13) Fanya mpango ili kukaa pamoja na wale uliowaalika, na uwe hakika kwamba wana Biblia na kitabu cha wimbo. Tutataka hasa kuchukua hatua ya kuwasalimu kwa shauku ndugu na dada wowote wasiotenda waliojitahidi kuhudhuria. Upendo wetu unaoonyesha kwamba tunapendezwa nao unaweza kuwasaidia waanze tena kushirikiana na kutaniko. (Luka 15:3-7) Kwenye tukio hilo takatifu zaidi, na tufanye yote tuwezayo ili kutia moyo wengine waambatane nasi katika kumtolea Yehova shukrani kwa ajili ya ‘fadhili zake zenye upendo za ajabu.’—Zab. 31:21.
[Maulizo ya Funzo]
1. Namna gani Yehova ametuonyesha fadhili zenye upendo?
2. Namna gani tunaweza kuonyesha shukrani yetu kwa Yehova?
3, 4. (a) Namna gani tunaweza kuiga roho ya ndugu zetu wa Liberia? (b) Unapanga kualika nani kwenye Ukumbusho?
5. Namna gani tunaweza kutia moyo wanafunzi wa Biblia kuhudhuria?
6. Kwa nini ni jambo la maana kuwakaribisha wageni kwenye Ukumbusho?