Tuwasaidie Ili Wapokee Ushahidi Zaidi
1 Tunapohubiri habari njema, mara nyingi tunakutana na watu wasioishi katika eneo letu au wanaosema lugha nyingine, kutia ndani lugha ya ishara. Wengine ambao tulikuwa tukizungumza nao wanaweza kuhamia mbali na eneo letu. Namna gani tunaweza kufanya mipango ili watu hao waendelee kupokea ushahidi zaidi? Kwa kutumia fomu Intérêt à suivre dans une langue étrangère (S-70a) inayopatikana sasa katika makutaniko yetu. Baadaye tutatumia fomu Veuillez suivre l’intérêt (S-43).
2 Mara nyingi watu wanasikiliza kwa hamu zaidi habari njema inapotolewa katika lugha yao ya asili. (Mdo. 22:1, 2) Ni kwa sababu hiyo, katika visa vingi, tunapokutana na mtu anayesema lugha nyingine, tunapaswa kujaza fomu hiyo hata ikiwa mtu haonyeshi kupendezwa na ujumbe wa Ufalme. Hata hivyo, mahali ambapo kuna sehemu kubwa ya watu wanaosema lugha ya kigeni na wanaopokea kwa ukawaida ushahidi katika lugha yao, haitakuwa lazima kujaza fomu isipokuwa tu wakati kupendezwa kunapoonyeshwa.
3 Kujaza Fomu: Kwa busara, jitahidi kupata jina la mtu, anwani yake, na namba yake ya simu. Onyesha ni kwa kiasi gani mtu alivyopendezwa, wakati anaweza kupatikana, kichapo ambacho umemwachia au ameomba, na lugha ambayo mtu huyo anasikia vizuri zaidi. Baada ya kujaza fomu, uipelekee mara moja mwandishi wa kutaniko, ambaye ataituma kwenye kikundi au kutaniko linaloweza kushughulikia mtu huyo.
4 Kuituma Fomu: Ikiwa mwandishi hajui kikundi au kutaniko ambalo linapaswa kupokea fomu hiyo au hana anwani ya kutaniko au kikundi, basi anaweza kuipigia simu Idara ya Eneo kwenye ofisi ya tawi ili kupata habari anayohitaji. Si lazima tena kumjulisha mwangalizi wa mji unapotuma fomu.
5 Wakati kikundi au kutaniko linapokea fomu Intérêt à suivre dans une langue étrangère yenye kujazwa, litachukua mipango ili kumtembelea mtu huyo haraka. Tunapotimiza sehemu yetu, tunaweza kuwa hakika kwamba Yehova atafungua mioyo ya wale ‘walio na mwelekeo unaofaa kwa ajili ya uzima wa milele.’—Mdo. 13:48.