Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 2/05 uku. 6
  • Tuwasaidie Ili Wapokee Ushahidi Zaidi

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tuwasaidie Ili Wapokee Ushahidi Zaidi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tuhubirie Watu Wanaozungumza Luga ya Kigeni
    Huduma Yetu ya Ufalme—2009
  • Jinsi ya Kutumia Fomu Tafadhali Fuatia Upendezi (S-43)
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Njia Mbalimbali za Kuhubiri Habari Njema
    Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
  • Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri—Kuhubiri Mutu Mwenye Kuzungumuza Luga Ingine
    Huduma Yetu ya Ufalme—2015
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2005
km 2/05 uku. 6

Tuwasaidie Ili Wapokee Ushahidi Zaidi

1 Tunapohubiri habari njema, mara nyingi tunakutana na watu wasioishi katika eneo letu au wanaosema lugha nyingine, kutia ndani lugha ya ishara. Wengine ambao tulikuwa tukizungumza nao wanaweza kuhamia mbali na eneo letu. Namna gani tunaweza kufanya mipango ili watu hao waendelee kupokea ushahidi zaidi? Kwa kutumia fomu Intérêt à suivre dans une langue étrangère (S-70a) inayopatikana sasa katika makutaniko yetu. Baadaye tutatumia fomu Veuillez suivre l’intérêt (S-43).

2 Mara nyingi watu wanasikiliza kwa hamu zaidi habari njema inapotolewa katika lugha yao ya asili. (Mdo. 22:1, 2) Ni kwa sababu hiyo, katika visa vingi, tunapokutana na mtu anayesema lugha nyingine, tunapaswa kujaza fomu hiyo hata ikiwa mtu haonyeshi kupendezwa na ujumbe wa Ufalme. Hata hivyo, mahali ambapo kuna sehemu kubwa ya watu wanaosema lugha ya kigeni na wanaopokea kwa ukawaida ushahidi katika lugha yao, haitakuwa lazima kujaza fomu isipokuwa tu wakati kupendezwa kunapoonyeshwa.

3 Kujaza Fomu: Kwa busara, jitahidi kupata jina la mtu, anwani yake, na namba yake ya simu. Onyesha ni kwa kiasi gani mtu alivyopendezwa, wakati anaweza kupatikana, kichapo ambacho umemwachia au ameomba, na lugha ambayo mtu huyo anasikia vizuri zaidi. Baada ya kujaza fomu, uipelekee mara moja mwandishi wa kutaniko, ambaye ataituma kwenye kikundi au kutaniko linaloweza kushughulikia mtu huyo.

4 Kuituma Fomu: Ikiwa mwandishi hajui kikundi au kutaniko ambalo linapaswa kupokea fomu hiyo au hana anwani ya kutaniko au kikundi, basi anaweza kuipigia simu Idara ya Eneo kwenye ofisi ya tawi ili kupata habari anayohitaji. Si lazima tena kumjulisha mwangalizi wa mji unapotuma fomu.

5 Wakati kikundi au kutaniko linapokea fomu Intérêt à suivre dans une langue étrangère yenye kujazwa, litachukua mipango ili kumtembelea mtu huyo haraka. Tunapotimiza sehemu yetu, tunaweza kuwa hakika kwamba Yehova atafungua mioyo ya wale ‘walio na mwelekeo unaofaa kwa ajili ya uzima wa milele.’—Mdo. 13:48.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine