Saidieni Watoto Wenu Wafanye Maendeleo Katika Huduma
1 Wazazi Wakristo wana daraka nzito la kuzoeza watoto wao katika huduma kuanzia umri mchanga. Hilo linaweza kutimizwa katika njia nyingi. Watoto wengine wana uwezo wa kutaja moja kwa moja maneno ya andiko la Biblia lenye kufaa hata kabla ya kujifunza kusoma. Hilo linaweza kuwa na matokeo yenye nguvu sana kwa wasikilizaji. Watoto wanapokomaa, wanaweza hata kufanya mengi zaidi katika huduma. Ninyi wazazi mnawezaje kusaidia watoto wenu washiriki katika kutoa ushahidi? Labda mapendekezo yanayofuata yatazidi kusaidia.
2 Baada ya kutoa salamu, unaweza kusema:
◼“Mwana wangu, [jina lake], ana andiko lenye maana ambalo angependa usikilize.” Mtoto wako anaweza kusema: “Andiko hili katika kitabu cha Zaburi lilinifundisha jina la Mungu. [Mtoto anasoma au anataja moja kwa moja maneno ya Zaburi 83:18.] Magazeti haya yanazungumzia yale ambayo Yehova atatufanyia. Je, ninaweza kukuachia hayo?” Unaweza kumalizia mazungumzo kwa kueleza jinsi kazi ya ulimwenguni pote inavyotegemezwa.
3 Au unaweza kujaribu utoaji huu:
◼“Jambo. Ninafundisha binti yangu, [jina lake], kuhangaikia watu wengine. Angependa kushiriki pamoja nawe ujumbe mfupi wa Biblia.” Anaweza kusema hivi: “Njia moja ambayo katika hiyo ninapenda kusaidia watu ni kushiriki tumaini la Biblia kuhusu wakati ujao. [Mtoto anasoma au kutaja moja kwa moja maneno ya Ufunuo 21:4.] Magazeti haya yanaeleza mambo ambayo Ufalme wa Mungu utatufanyia. Ninafikiri kwamba utafurahi kuyasoma.”
4 Kutumia mara kwa mara utoaji ulio rahisi kunasaidia watoto kuwa na uhakika katika uwezo wao wa kushiriki ujumbe wa Ufalme. Kujizoeza vipindi vinavyokaza fikira juu ya kusema waziwazi na kwa sauti ya kutosha kutawatolea vifaa ili kusema katika hali mbalimbali. Kujitayarisha vizuri kimbele na kutoa pongezi kwa moyo mnyofu kutasaidia watoto kuonyesha imani yao.
5 Kwa kuwatia moyo namna hiyo, watoto wengi wamekuwa na sifa za kustahili kuwa wahubiri wasiobatizwa. Ni furaha kama nini kuona watoto wetu wakifanya maendeleo katika huduma ya Kikristo!—Zab. 148:12, 13.