Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 8/05 uku. 1
  • Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Namna ya Kusaidia Wanafunzi wa Biblia Wafikie Kubatizwa—Sehemu ya Pili
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Namna ya Kusaidia Wanafunzi wa Biblia Wafikie Kubatizwa—Sehemu ya Kwanza
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2005
km 8/05 uku. 1

Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo

Sehemu 12: Kusaidia Wanafunzi Kuanzisha na Kuongoza Mafunzo ya Biblia

1 Wakati wanafunzi wa Biblia wanapoanza kushiriki katika huduma ya shambani, wanaweza kuogopeshwa na wazo la kuanzisha na kuongoza wao wenyewe mafunzo ya Biblia. Tunawezaje kuwasaidia wasitawishe mtazamo unaofaa kuelekea sehemu hiyo ya maana ya huduma yetu?—Mt. 24:14; 28:19, 20.

2 Mwanafunzi wa Biblia atakapokuwa amestahili kuwa mhubiri asiyebatizwa, inaelekea kwamba yeye amekwisha kufaidika sana na Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Mazoezi anayopokea katika kutayarisha na kutoa migawo ya mwanafunzi itamsaidia kusitawisha ufundi mbalimbali wa kufundisha ambao unahitajiwa kwa ‘mfanyakazi asiye na lolote la kuonea aibu [haya], akilitumia sawasawa neno la kweli.’—2 Tim. 2:15.

3 Fundisha Kupitia Mfano Wako: Yesu alizoeza wanafunzi wake kwa kuwapa maagizo yaliyo wazi na kuwawekea mfano bora. Alisema: “Kila mtu aliyefundishwa kikamili atakuwa kama mwalimu wake.” (Luka 6:40) Kumwiga Yesu kwa kuweka mfano unaofaa katika huduma yako ni jambo la maana. Mwanafunzi anapotazama mfano wako katika huduma, ataelewa kwamba mradi katika kufanya ziara za kurudia ni kuanzisha mafunzo ya Biblia.

4 Umuelezee mwanafunzi kwamba tunapotolea mwenye nyumba funzo, kwa kawaida si lazima kumfafanulia kirefu mpango wa funzo. Mara nyingi ni jambo bora zaidi kuonyesha tu jinsi ya kuongoza funzo kwa kutumia fungu moja au mafungu mawili kutoka kitabu cha funzo. Mapendekezo yenye kufaa ili kufanya hivyo yanaweza kupatikana kwenye ukurasa wa 8 wa nakala hii na kwenye ukurasa wa 6 wa Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2002.

5 Inapofaa, alika mwanafunzi aambatane nawe au na mhubiri mwengine mwenye uzoefu kwenye mafunzo mengine ya Biblia. Anaweza kushiriki katika kutoa maelezo kwenye fungu fulani au andiko fulani la msingi. Hivyo, kwa kuwa mtazamaji, mwanafunzi atajifunza mengi kuhusu kuongoza mafunzo ya Biblia yenye kuendelea. (Met. 27:17; 2 Tim. 2:2) Umpongeze, na muzungumze jinsi anavyoweza kufanya maendeleo.

6 Kuzoeza wahubiri wapya kuwa walimu wa Neno la Mungu kutawatolea vifaa kwa ajili ya “kazi njema” ya kuanzisha na kuongoza wao wenyewe mafunzo. (2 Tim. 3:17) Ni jambo lenye kupendeza kabisa kutumika pamoja nao katika kueneza mwaliko huu wenye upendo: “Na yeyote anayetaka achukue maji ya uzima bure.”—Ufu. 22:17.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine