Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 7/04 uku. 1
  • Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo ya Mlangoni na kwa Njia ya Simu
    Huduma Yetu ya Ufalme—2006
  • Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Biblia Inafundisha— Kitabu Chetu cha Lazima cha Kujifunzia Biblia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2006
  • Namna ya Kusaidia Wanafunzi wa Biblia Wafikie Kubatizwa—Sehemu ya Kwanza
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 7/04 uku. 1

Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo

Sehemu 1: Funzo la Biblia Ni Nini?

1 Ulimwenguni pote, karibu mafunzo ya Biblia milioni sita ni yenye kuongozwa na watu wa Mungu kila mwezi. Kwa kutumia njia za kufundisha zenye matokeo, tunaweza kusaidia wanafunzi wa Biblia hao kufanya maendeleo mpaka kufikia wakfu na ubatizo, na kuwa “na sifa za kustahili vya kutosha kufundisha wengine.” (2 Tim. 2:2) Je, ungependa kusaidia mwanafunzi wako ili afanye maendeleo ya namna hiyo? Kuanzia na toleo hili, Huduma Yetu ya Ufalme itatoa mfululizo wa makala zitakazofafanua sehemu za msingi katika kuongoza mafunzo ya Biblia yenye maendeleo.

2 Wakati wa Kutoa Ripoti ya Funzo la Biblia: Ikiwa una mazungumzo, hata mafupi, ya Biblia pamoja na mtu mwenye kupendezwa, na ikiwa unazungumzia kwa ukawaida na kwa utaratibu habari fulani ukitumia Biblia na kimoja cha vichapo vinavyopendekezwa, unaongoza funzo la Biblia. Hilo ni kweli hata ikiwa funzo linafanyika mlangoni au kwa njia ya simu. Funzo linaweza kuripotiwa ikiwa limeongozwa mara mbili baada ya kumwonyesha mtu jinsi ya kujifunza na ikiwa kuna sababu inayosadikisha kwamba funzo hilo halitakatizwa.

3 Broshua Anataka na kitabu Ujuzi ndivyo vichapo vinavyotumiwa ili kuongoza mafunzo mengi ya Biblia. Baada ya kumaliza vichapo hivyo, ikiwa ni wazi kwamba mtu ni mwenye kufanya maendeleo, hata ingawa ni polepole, na kwamba ni mwenye kuonyesha zaidi uthamini kwa yale anayojifunza, basi mnaweza kuendelea kujifunza kitabu Mwabudu Mungu. Broshua Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu! inaweza kutumiwa ili kujifunza na watu wenye elimu ndogo au uwezo mdogo wa kusoma.

4 Kazi ya kuongoza mafunzo ya Biblia imekuwa yenye matokeo katika kusaidia mamilioni ya watu kuwa wanafunzi wa kweli wa Yesu Kristo. (Mt. 28:19, 20) Kwa kutumia mapendekezo yanayotolewa katika makala yatakayofuata ya mfululizo huu, unaweza kuongoza funzo la Biblia lenye maendeleo.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine