Wahubiri Wapendwa wa Ufalme:
Mwanzoni mwa mwaka mpya wa utumishi, mzunguko mmoja uliundwa katika eneo la ofisi ya tawi la Kongo. Eneo la ofisi ya tawi letu lina sasa mizunguko 137 na wilaya 12.
Kazi kubwa imefanywa ili kupanga Mikusanyiko ya Wilaya 92 na programu nyingine ndogo 7 katika eneo lote la ofisi ya tawi. Mafundisho yalitolewa katika lugha 11, kutia ndani lugha ya ishara, programu zingine zikiwa zenye kufupishwa. Tunawapongeza nyinyi nyote ndugu mliofanya safari ndefu ili kuhudhuria mpango huu wa maana wa kiroho.—Kum. 31:12.
Kumepita mwaka mmoja hivi tangu uanzishwe ujenzi wa Makao ya Wanabetheli yenye majengo matatu yenye orofa mbili katika uwanja wa Betheli ya Kinshasa. Majengo hayo yatakuwa na jumla ya vyumba vipya 84. Kazi ya kwanza ilihusisha kujenga msingi wa majengo hayo matatu. Jumla ya matoni 16000 au malori 1000 ya changarawe (mawe madogo-madogo) ililetwa kwenye uwanja, ili kuinua na kufanya mahali pa kujenga msingi pawe pagumu.
Kampuni moja ya ujenzi ndio inayojenga makao hayo mapya. Ndugu wanaotumika katika Idara ya Ujenzi ya Betheli ndio wanaofanya Kadirio la Ubora wa Kazi kuhusu majengo yote. Wanashirikiana vizuri sana na wafanyakazi wa kampuni hiyo. Mmoja wa wafanyakazi wao alisema: “Kituo hiki cha ujenzi ni tofauti. Watu wenu wote wanatusalimu, wasimamizi wenu wanasalimu wafanyakazi wetu wote, jambo hilo si la kawaida kwenye vituo vingine vya ujenzi.” Mwingine alisema: “Mungu iko pamoja nanyi kabisa kwa kuwa muda wote mgumu tulipokuwa tukijenga msingi, mvua haikunyesha sana kama kawaida.”
Kazi ya ujenzi wa kuta ni yenye kuendelea kulingana na programu jinsi ilivyopangwa. Kwa wakati unaofaa, majengo hayo matatu yatakapokamilishwa, familia ya Betheli ya Kinshasa itakuwa na nafasi bora itakayoiwezesha kutumikia ndugu wote katika Kongo. Utendaji wote huo wenye bidii katika kuendeleza faida za Ufalme ni wenye kupongezwa! Tegemezo lenu la ukarimu la kifedha kuhusu kazi hii ni lenye kuthaminiwa sana. (Met. 3:9, 10) Yehova na abariki jitihada zetu zenye umoja ili ‘kutumikia kwa ajili ya sifa ya utukufu wake.’—Efe. 1:12.
Ndugu zenu,
Ofisi ya Tawi la Kongo