Wahubiri Wapendwa wa Ufalme:
Tunafurahi kuona maendeleo ya kazi katika eneo la tawi letu katika mwaka wa utumishi wa 2007! Katika Congo-Kinshasa, tulifikia hesabu kubwa ya wahubiri 138,273 na mapainia wa kawaida 10,765 mwezi wa 1 wa mwaka huo. Katika Congo-Brazzaville, tulifikia hesabu kubwa ya wahubiri 5,406 mwezi wa 4, 2007. Katika miezi minane ya kwanza ya mwaka wa utumishi wa 2007, Wanabetheli 33 wamealikwa ili kutusaidia kwenye tawi. Katika idara mbalimbali, tuna lazima ya wafanyakazi wenye kujitolea wanaostahili, zaidi sana kwa ajili ya kazi ya kutafsiri.
Karibu milioni 8 za trakti Habari ya Ufalme Na. 37 yenye kichwa: “Mwisho wa Dini ya Uongo Unakaribia!” ziligawanywa katika eneo lote la tawi letu. Ripoti mbalimbali zinaonyesha kwamba, kisha kupokea na kusoma trakti, watu waliwashukuru Mashahidi wa Yehova kwa sababu ujumbe huo uliwafungua macho. Wameelewa kwamba ni jambo la maana sana kutambua dini ya kweli. Wengi walihuzuria mikutano na walikubali kujifunza Biblia.
Kusudi la kampanye hizo ni kusaidia watu wenye mioyo minyofu kujifunza yale ambayo Biblia inafundisha kabisa. (Mt. 28:19, 20) Unapohubiri, kumbuka kuandika mambo fulani kuhusu kila mtu anayeonyesha kupendezwa na umrudilie ukiwa na kusudi la kuanzisha naye funzo la Biblia na kuendelea kujifunza na wale walio na “mwelekeo unaofaa kwa ajili ya uzima wa milele.” (Mdo. 13:48) Sisi ni wenye furaha kutumika nanyi kwa kuungana mkono katika kazi hii iliyo ya maana na tunawatumia salamu zetu changamfu za upendo wa Kikristo.
Ndugu zenu,
Betheli ya Congo-Kinshasa