Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 9/07 uku. 1
  • Wahubiri Wapendwa wa Ufalme:

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Wahubiri Wapendwa wa Ufalme:
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Ni Kazi Gani Zinafanywa ku Biro ya Tawi?
    Ni Nani Wanafanya Mapenzi ya Yehova Leo?
  • Wahubiri Wapendwa wa Ufalme:
    Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Namna ya Kupanua Utumishi Wako
    Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
  • Habari Za Kitheokrasi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2007
km 9/07 uku. 1

Wahubiri Wapendwa wa Ufalme:

Tunafurahi kuona maendeleo ya kazi katika eneo la tawi letu katika mwaka wa utumishi wa 2007! Katika Congo-Kinshasa, tulifikia hesabu kubwa ya wahubiri 138,273 na mapainia wa kawaida 10,765 mwezi wa 1 wa mwaka huo. Katika Congo-Brazzaville, tulifikia hesabu kubwa ya wahubiri 5,406 mwezi wa 4, 2007. Katika miezi minane ya kwanza ya mwaka wa utumishi wa 2007, Wanabetheli 33 wamealikwa ili kutusaidia kwenye tawi. Katika idara mbalimbali, tuna lazima ya wafanyakazi wenye kujitolea wanaostahili, zaidi sana kwa ajili ya kazi ya kutafsiri.

Karibu milioni 8 za trakti Habari ya Ufalme Na. 37 yenye kichwa: “Mwisho wa Dini ya Uongo Unakaribia!” ziligawanywa katika eneo lote la tawi letu. Ripoti mbalimbali zinaonyesha kwamba, kisha kupokea na kusoma trakti, watu waliwashukuru Mashahidi wa Yehova kwa sababu ujumbe huo uliwafungua macho. Wameelewa kwamba ni jambo la maana sana kutambua dini ya kweli. Wengi walihuzuria mikutano na walikubali kujifunza Biblia.

Kusudi la kampanye hizo ni kusaidia watu wenye mioyo minyofu kujifunza yale ambayo Biblia inafundisha kabisa. (Mt. 28:19, 20) Unapohubiri, kumbuka kuandika mambo fulani kuhusu kila mtu anayeonyesha kupendezwa na umrudilie ukiwa na kusudi la kuanzisha naye funzo la Biblia na kuendelea kujifunza na wale walio na “mwelekeo unaofaa kwa ajili ya uzima wa milele.” (Mdo. 13:48) Sisi ni wenye furaha kutumika nanyi kwa kuungana mkono katika kazi hii iliyo ya maana na tunawatumia salamu zetu changamfu za upendo wa Kikristo.

Ndugu zenu,

Betheli ya Congo-Kinshasa

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine