Habari Za Kitheokrasi
◼ Armenia: Kulingana na ripoti ya Desemba, kila mmoja wa wale wahubiri 4, 741 alipitisha kwa wastani saa 16 katika huduma. Kilele hicho kipya cha wahubiri ni sawa na ongezeko la asilimia 17 kwa kulinganisha na wastani wa mwaka uliopita.
◼ Chili: Marekebisho ya kiwango cha saa za mapainia yalipokewa kwa shauku, kama inavyoonyeshwa na kilele kisicho na kifani cha mapainia wa kawaida 4, 351 mnamo Januari. Zaidi ya hayo, kulikuwako mapainia wasaidizi 5, 175; hayo yalikuwa matokeo bora zaidi katika mwaka wa utumishi.
◼ Ukrainia: Mnamo Januari, asilimia 12 ya wale wahubiri 100, 129 waliotoa ripoti walikuwa katika aina moja au nyingine ya utumishi wa wakati wote. Ukrainia ilikuwa na mapainia wa kawaida 5, 516, hicho kikiwa kilele mfululizo cha 27, na mapainia wasaidizi 6, 468.