Urekebishaji wa Idadi ya Saa Zinazoombwa kwa Mapainia
1 Sote tunathamini kazi ngumu wanayotimiza mapainia wa kawaida na mapainia wasaidizi katika kutaniko. Hata wakati eneo ni dogo na lenye kutembelewa kikamili kwa kawaida, mapainia hutoa kielelezo chema cha bidii katika utumishi wa Ufalme. Wanatia moyo wahubiri wote waendelee kujitoa katika kutafuta wale walio na “mwelekeo ufaao.”—Mdo. 13:48.
2 Sosaiti inatambua kwamba mapainia hupambana na matatizo mengi zaidi na zaidi; tatizo kubwa ni kupata kazi ya muda iwezayo kufanya iwezekane kwa mapainia hao kutosheleza ifaavyo mahitaji yao na kubaki katika utumishi wa wakati wote. Tena, kwa sababu ya hali ya kiuchumi ya sasa, imekuwa vigumu zaidi na zaidi kwa wahubiri wengine katika nchi nyingi kuja kwenye mstari wa mapainia, ingawaje wana tamaa kubwa ya kufanya hivyo. Miezi hii iliyopita, mambo hayo na mengineyo yalifikiriwa kwa makini.
3 Kwa sababu hiyo, Sosaiti inapunguza kiwango cha saa kwa mapainia wa kawaida na wasaidizi. Kuanzia mwaka 1999, kiwango cha saa 70 ndicho kinachoombwa kwa mapainia wa kawaida kila mwezi, ni kusema jumla ya saa 840 kwa mwaka. Kiwango cha saa 50 kitakuwa kikiombwa kila mwezi kwa mapainia wasaidizi. Kwa mapainia wa pekee na wamishonari, kiwango cha saa kinabaki bila kubadilika, kwa kuwa mipango ya Sosaiti hufanya iwezekane kwao kutosheleza mahitaji ya lazima. Wanaweza hivyo kukaza fikira kikamili zaidi juu ya kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi.
4 Tunatumaini kwamba urekebishaji huo wa kiwango cha saa utasaidia mapainia wengi zaidi wadumu katika pendeleo lao la utumishi lenye kupendwa sana. Jambo hilo lingepaswa vilevile kuwapa wahubiri wengi zaidi uwezekano wa kuwa mapainia wasaidizi au wa kawaida. Itakuwa baraka kama nini kwa kila mmoja katika kutaniko!