Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 8/06 uku. 1
  • Amkeni! ya Pekee Itakayokaziwa Katika Mwezi wa Kenda

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Amkeni! ya Pekee Itakayokaziwa Katika Mwezi wa Kenda
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2006
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Amkeni! ya Pekee ya Kutolea Watu Katika Mwezi wa 11!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Jinsi ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia na Watu Tuliotolea Magazeti
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Chagua Makala Kwa Kulenga Kupendezwa Kwa Watu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Tia Nguvu Imani Yako Katika Muumbaji
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2006
km 8/06 uku. 1

Amkeni! ya Pekee Itakayokaziwa Katika Mwezi wa Kenda

1 Karibu kila mtu anafurahia kusikia ndege wakiimba na kuona hali nzuri ya jua linapotua. Hata hivyo, wengi hawakubali kwamba vitu hivyo viliumbwa na Baba mwenye upendo aliye mbinguni. Tutakuwa na nafasi ya pekee ya kutoa ushahidi kuhusu uumbaji wa Yehova kwa kugawanya Amkeni! hiyo ya pekee. (Isa. 40:28; 43:10) Amkeni! hiyo inazungumzia tu habari yenye kusema: ‘Je, Kuna Muumba?’

2 Katika Eneo: Kama inawezekana, fanya mpango wa kuhubiri nyumba kwa nyumba pamoja na kutaniko kila Siku ya Posho. Kwa kweli, unaweza kutolea watu gazeti hilo la pekee wakati wowote katika juma. Walimu, na wengine wanaohusika na mambo ya kufundisha watapendezwa hasa na gazeti hilo. Kwa hiyo, mipango ya pekee inaweza kufanywa ili kuwatembelea watu kama hao wanaopatikana katika eneo lenu.

3 Ikiwa mtu anapendezwa, umwachie ulizo ambalo utajibia utakapomurudilia. Kwa mfano, unaweza kumuuliza kwa nini Muumba mwenye upendo anaruhusu watu wateseke sana. Kisha, utakaporudia, unaweza kuchunguza naye sura ya 1 au sura ya 11 ya kitabu Biblia Inafundisha. Au unaweza kuchagua ulizo linalozungumzia kusudi la Muumba kuhusu dunia na kisha kuchunguza sura ya 3.

4 Somoni: Ikiwa wewe ni mwanafunzi, unaweza kuwapatia walimu na wanafunzi wenzako zawadi ya Amkeni! hiyo ya pekee. Sivyo? Ukitia tu gazeti moja kwenye meza yako ya kuandikia, jambo hilo linaweza kufanya wengine wakuulize maulizo kuhusu mambo tunayoamini. Kwa hiyo, itawezekana uwe na nafasi ya kutumia habari zinazopatikana katika gazeti hilo utakapoitetea imani yako katika mazungumzo ya somoni na wakati mtakapoombwa kuandika kuhusu jambo fulani linalohusu uumbaji. Ili kukusaidia kufanya hivyo, gazeti hilo lina habari inayosema “Vijana Wanauliza,” yenye kichwa ‘Namna Gani Ninaweza Kutetea Mambo Ninayoamini Kuhusu Uumbaji?’

5 Yehova anastahili kupewa heshima na utukufu kwa sababu ya vitu alivyoumba. (Ufu. 4:11) Tunaweza kuonyesha kwamba tunamheshimu Muumba wetu na kwamba tunapenda kuwasaidia wengine wafanye hivyo kwa kuwatolea watu kwa shauku Amkeni! ya mwezi wa Kenda.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine