Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 12/06 uku. 6
  • Kuonyesha Roho ya Kujitolea Kunaleta Baraka

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kuonyesha Roho ya Kujitolea Kunaleta Baraka
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2006
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Usaidie Katika Kazi ya Ujenzi
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2022
  • Unaweza Kujitolea?
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2020
  • Mipango ya Ofisi ya Tawi Kuhusu Ujenzi Ni Sehemu ya Maana ya Utumishi Mtakatifu
    Huduma Yetu ya Ufalme—2006
  • Roho Yako ya Kujitolea Imuletee Yehova Sifa!
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2017
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2006
km 12/06 uku. 6

Kuonyesha Roho ya Kujitolea Kunaleta Baraka

1 Goliathi alipoyatukana majeshi ya vita ya Israeli, hakuna hata askari mmoja aliyejitolea ili kumpiganisha; mchungaji mmoja kijana asiyezoezwa katika mambo ya vita ndiye aliyejitolea kupigana naye. (1 Sam. 17:32) Wayahudi waliohamishwa waliporudi Yerusalemu na waliposhindwa kujenga kuta, ni mnyweshaji wa Mfalme wa Uajemi aliyejitolea kuacha cheo chake chenye heshima katika nyumba ya Mfalme na kusafiri Yerusalemu ili kupanga kazi ya ujenzi. (Neh. 2:5) Yehova alibariki wanaume hao wawili, Daudi na Nehemia, kwa sababu ya roho walioonyesha.—1 Sam. 17:45, 50; Neh. 6:15, 16.

2 Leo, roho ya kujitolea inakosekana katika ulimwengu. Katika hizi “siku za mwisho,” watu wana mambo mengi sana ya kufanya maishani, na wengi ni “wenye kujipenda wenyewe.” (2 Tim. 3:1, 2) Ni rahisi sana mtu kuhangaikia sana mambo yake mwenyewe hivi kwamba akose kutumia nafasi zinazopatikana ili kujitolea kwa ajili ya wengine wakati kuna uhitaji wa kuwasaidia. Hata hivyo, tukiwa Wakristo, tunataka kufuata mfano wa Yesu, aliyechukua hatua ya kusaidia wengine. (Yoh. 5:5-9; 13:12-15; 1 Pet. 2:21) Namna gani tunaweza kuonyesha roho ya kujitolea, na ni baraka gani tutakazopata kwa kufanya hivyo?

3 Kujitolea kwa Ajili ya Ndugu Zetu: Tunaweza kupatia wengine “zawadi ya kiroho” kwa kujitolea kutoa maelezo wakati wa sehemu za mkutano zinazoomba wasikilizaji washiriki. (Rom. 1:11) Kutoa maelezo kunamletea Yehova utukufu, kunakazia sana kweli katika akili na moyo wetu na kunafanya tufurahie zaidi mikutano. (Zab. 26:12) Tunaweza pia kujitolea ili kutoa hotuba kwenye Shule ya Huduma ya Kitheokrasi wakati yule aliyepewa mgawo huo hayupo. Jambo hilo litatusaidia kufanya uwezo wetu wa kufundisha uwe bora.

4 Ndugu wanaweza kuonyesha roho ya kujitolea kwa kujikaza kutimiza sifa ili wachukue madaraka katika kutaniko. (Isa. 32:2; 1 Tim. 3:1) Kwa kujitolea kufanya kazi katika idara mbalimbali, wote wanaweza kusaidia ili mikusanyiko ya mzunguko, ya pekee ya siku moja na ya wilaya iendeshwe vizuri. Tunapojitolea kuhubiri pamoja na waangalizi wasafiri au kuwatolea chakula, jambo hilo linafanya kuwe “ubadilishanaji wa kitia-moyo.” (Rom. 1:12) Tunapata furaha na tunakubaliwa na Yehova tunapojitolea ili kusaidia watoto wasio na baba, wajane, wagonjwa na walemavu, mama walio na watoto wadogo na watu wengine katika kutaniko.—Met. 19:17; Mdo. 20:35.

5 Namna nyingine ya kujitolea ni kutoa wakati wetu na nguvu zetu ili kusaidia kusafisha na kutunza Jumba la Ufalme. Zaidi ya hilo, kwa kuwa watu wengi wanakuja katika kweli, kuna lazima yenye kuongezeka ya Majumba ya Ufalme na watu wenye kujitolea ili kujenga Majumba hayo. Mume na muke mmoja walijitolea kusaidia katika Ofisi ya Tawi Inayohusika na Majumba ya Ufalme ya mahali pao ijapokuwa hawakukuwa na ufundi katika mambo ya ujenzi. Mwishowe, walipewa mazoezi na sasa wanasaidia katika kazi ya kutengeneza matofali. Muke alieleza: “Kutumika bega kwa bega pamoja na wengine kumetufanya tuwe na marafiki wa karibu. Mwishoni mwa siku, tunakuwa wenye kuchoka kimwili, lakini tuna nguvu kiroho.”

6 Kuonyesha Roho ya Kujitolea kwa Kuhubiri: Kazi ya kuhubiri Ufalme ndiyo kazi ya kujitolea iliyo ya maana sana ambayo tunaweza kufanya leo. Watu wanakuwa na kusudi maishani na wanapata nguvu ya kushinda tabia mbaya wakati tunawasaidia kuelewa na kutumia mashauri ya Biblia. Wanajifunza tumaini bora la Biblia kuhusu wakati ujao. Kwa kufundisha watu Biblia, tunatimiza kwa furaha kazi ya kujitolea inayoletea wengine baraka za kudumu. (Yoh. 17:3; 1 Tim. 4:16) Labda hali zetu zinaweza kuturuhusu ili kushiriki zaidi katika kazi hiyo kwa kutumika kama painia msaidizi au painia wa kawaida, kwa kuhamia mahali ambapo kuna lazima kubwa ya wahubiri au kwa kujifunza luga nyingine.

7 Mfalme Daudi alitabiri kwamba wakati Masihi atakapoanza kutawala, “watu wa Mungu watajitoa kwa hiari.” (Zab. 110:3, Rbi8-F, maelezo yaliyo chini ya ukurasa) Kwa kuwa Yehova anaharakisha mavuno ya mwisho ya kiroho, kuna kazi nyingi zinazoomba kujitolea. (Isa. 60:22) Je, umesema: “Mimi hapa! Nitume mimi”? (Isa. 6:8) Kwa kweli, kwa kuonyesha roho ya kujitolea, tunamfurahisha Yehova na tunavuna zawadi nyingi.

[Maulizo ya Funzo]

1. Namna gani Daudi na Nehemia walionyesha roho ya kujitolea?

2. Kwa nini Wakristo wanapaswa kuonyesha roho ya kujitolea?

3. Namna gani roho ya kujitolea inasaidia wakati wa mikutano ya kutaniko?

4. Ni kwa njia gani zingine tunaweza kuonyesha roho ya kujitolea?

5. Ni mambo gani kuhusu Jumba la Ufalme yanayoomba roho ya kujitolea?

6. Kwa nini kazi ya kuhubiri ndiyo kazi ya kujitolea iliyo ya maana sana ambayo tunaweza kufanya?

7. Kwa nini kujitolea ni kwa maana zaidi sana leo?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine