Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 3/07 uku. 6
  • “Ungejibuje?”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • “Ungejibuje?”
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Habari za Kufanana na Zile
  • (1) Kutumia Maulizo, (2) Andiko, na (3) Sura Ili Kuanzisha Funzo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2006
  • Habari Mupya ili Kuanzisha Mazungumuzo
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2016
  • Kutilia Biblia Mkazo Zaidi!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Je, Unatumia Sehemu Zake Zote?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2007
km 3/07 uku. 6

“Ungejibuje?”

1 Je, unapenda Neno la Mungu lakini una magumu ya kukumbuka mambo madogo-madogo kuhusu masimulizi ya Biblia au kukumbuka mahali ambapo maneno fulani yanapatikana katika Maandiko? Je, ungependa watoto wako waelewe vizuri mafundisho ya mwanzo-mwanzo ya Biblia? Sehemu “Ungejibuje?” yenye kuchapishwa kila mwezi kwenye ukurasa wa 31 wa Amkeni! inaweza kusaidia vijana na watu wazima pia ili kuelewa vizuri Neno la Mungu.—Mdo. 17:11.

2 Namna gani unaweza kutumia vizuri sehemu hiyo? Amkeni! ya mwezi wa 1, 2006, ilitoa mapendekezo yafuatayo: “Hebu tazama ukurasa wa 31 . . . Sehemu fulani za ukurasa huu zitawavutia wasomaji wachanga; nyingine zitachangamsha akili ya watu wenye ujuzi zaidi wa Biblia. Sehemu ‘Ilitukia Lini?’ itakusaidia uwe na chati ya tarehe inayoonyesha kipindi cha wakati ambacho watu wanaotajwa katika Biblia waliishi na mambo muhimu yaliyotukia wakati huo. Ingawa majibu ya sehemu ‘Kutoka Katika Toleo Hili’ yatapatikana katika gazeti lote, majibu ya mengi ya maswali yatachapishwa yakiwa juu-chini katika ukurasa fulani. Mbona usifanye utafiti fulani kabla ya kusoma majibu hayo kisha uwaeleze wengine yale ambayo umejifunza? Unaweza pia kuzungumzia sehemu hii mpya, ‘Ungejibuje?’ ukiwa na familia yako au na kikundi chochote unachoshirikiana nacho.”

3 Kwa kweli, familia nyingi zinafurahia kutumia sehemu hii katika mazungumzo ya funzo lao la familia. Mama mmoja anaandika hivi: “Mimi na mume wangu tulifikiri kwamba ni jambo nzuri kutia sehemu ‘Watoto Watafute Picha’ katika mazungumzo ya funzo letu la familia ili kulifanya lichochee na lipendeze sana binti wetu mwenye umri wa miaka tatu. Tunafurahia sana kumwangalia akichukua kwa furaha Amkeni! lake na akifungua kurasa zote mpaka kupata jambo analotafuta.” Baba mmoja katika Brésil alisema hivi: “Mimi na mwana wangu mwenye umri wa miaka saba tunafurahia sana sehemu hii ya Amkeni! Ilisaidia Moises ili kuwa mwangalifu, kutafuta Maandiko, kuelewa maana ya picha na tarehe mbalimbali.” Ashley, aliye na umri wa miaka minane anaandika: “Asanteni kwa sehemu ‘Ungejibuje?’ iliyo kwenye ukurasa wa mwisho wa Amkeni! Ninajifunza mambo mengi ya Biblia kupitia sehemu hiyo.”

4 Kwa nini usitumie mara kwa mara sehemu “Ungejibuje?” katika mazungumzo ya funzo lenu la familia? Unaweza kutumia Index au Watchtower Library kwenye CD-ROM ili kutafuta majibu ya maulizo fulani yaliyo magumu zaidi. Kwa kufanya hivyo, utafundisha watoto wako namna ya kutafuta majibu wao wenyewe katika vitabu. Ikiwa una watoto wakubwa, unaweza kuwapa, kabla ya kufanya funzo la familia, kazi iliyo ngumu ya kutafuta majibu ya maulizo “Mimi ni Nani?” au “Ilitukia Lini?”. Kisha hapo, wakati wa funzo la familia wanaweza kuchangia na wengine matokeo ya mambo ambayo walitafuta. Kutumia ukurasa huo inavyofaa ni njia moja ambayo wazazi wanaweza kutumia ili kukazia Neno la Mungu katika watoto wao, na kuwasaidia kujua “maandishi matakatifu” tangu utotoni.—2 Tim. 3:15; Kum. 6:7.

[Maulizo ya Funzo]

1. Wengi kati yetu wana magumu gani?

2. Namna gani unaweza kutumia mambo mbalimbali ya sehemu “Ungejibuje?”

3. Namna gani familia fulani zimepata faida kupitia sehemu hii, na ni mambo gani ya sehemu hii unayofurahia zaidi?

4. Namna gani familia inaweza kutumia sehemu hii kati ya mambo wanayozungumzia katika funzo lao la familia?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine