Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 8/07 uku. 1
  • Tunafurahia Sana Mapendeleo Yetu!

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tunafurahia Sana Mapendeleo Yetu!
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Furahia Pendeleo Lako la Kutumika Pamoja na Yehova
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Barua ya Baraza Yenye Kuongoza
    Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
  • Yohana Mubatizaji​—Mufano Wake Unaweza Kutusaidia Tuendelee Kuwa na Furaha
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
  • Kuhubiri Ufalme—Pendeleo Lenye Thamani
    Huduma Yetu ya Ufalme—2005
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2007
km 8/07 uku. 1

Tunafurahia Sana Mapendeleo Yetu!

1 Muda wote ambao wanadamu wamepata kuishi, Yehova amewatolea watumishi wake mapendeleo mengi tofauti. Amewapa mapendeleo bila kujali ikiwa ni mwanamume au mwanamuke, miaka au hali yao ya maisha. (Luka 1:41, 42; Mdo. 7:46; Flp. 1:29) Ni mapendeleo gani anayotutolea leo?

2 Mapendeleo Yetu Fulani: Tuna pendeleo la kufundishwa na Yehova. (Mt. 13:11, 15) Tunafurahia pendeleo lingine la kumsifu Yehova kupitia maelezo yetu wakati wa mikutano ya kutaniko. (Zab. 35:18) Tunapopata pendeleo la kutoa maelezo, tunafanya hivyo kwa uchangamfu. Vivyo hivyo, ikiwa tunaona kila mgawo tunaopewa katika kutaniko kuwa pendeleo, tutafanya kadiri tuwezavyo ili kuutimiza vizuri. Je, tunashiriki kwa ukawaida katika pendeleo la kusafisha Jumba la Ufalme na kulitunza vizuri?

3 Ijapokuwa mamilioni ya watu wanajiuliza ikiwa Mungu anasikia sala zao, sisi tuna pendeleo la kujua kwamba sala zetu zinasikiwa na Mtu wa maana zaidi ulimwenguni. (Met. 15:29) Yehova mwenyewe anasikiliza sala za watumishi wake. (1 Pet. 3:12) Haweki mipaka kuhusu mara ngapi tunapaswa kumkaribia. Kusali “kila wakati,” ni zawadi yenye kufurahisha kabisa tuliyo nayo! Efe. 6:18.

4 “Wafanyakazi Wenzi wa Mungu”: Pendeleo moja lililo nzuri zaidi kati ya mapendeleo yetu ni lile la kutangaza habari njema za Ufalme wa Mungu tukiwa “wafanyakazi wenzi wa Mungu.” (1 Kor. 3:9) Hiyo ni kazi inayoleta kutosheka na ni yenye kutia nguvu. (Yoh. 4:34) Yehova hahitaji kutumia wanadamu ili kutimiza kazi yake, lakini anatutolea mgawo huo kwa sababu anatupenda. (Luka 19:39, 40) Katika kutoa mgawo huo, Yehova hafanye hivyo ovyoovyo. Wale wanaoshiriki katika utumishi wa watu wote wanapaswa kutimiza na kuendelea kuwa na sifa fulani za kiroho. (Isa. 52:11) Je, tunaonyesha kwamba tunafurahia pendeleo hilo kwa kufanya kazi ya kuhubiri iwe sehemu ya maana katika programu yetu ya kila juma?

5 Mapendeleo kutoka kwa Yehova yanafanya maisha yetu yawe yenye kutosheleza. (Met. 10:22) Usipuuze hata kidogo mapendeleo hayo! Tunapoonyesha kwamba tunafurahia kwelikweli mapendeleo yetu ya utumishi, tunamfurahisha Baba yetu wa mbinguni, Mtoaji wa “kila zawadi njema na kila tuzo kamilifu.”—Yak. 1:17.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine