Programu Mpya ya Mkusanyiko wa Pekee wa Siku Moja
Kichwa cha programu ya mkusanyiko wa pekee wa siku moja wa mwaka wa utumishi wa 2008 ni “Sisi Ni Udongo—Yehova Ni Mfinyanzi Wetu,” kinategemea andiko la Isaya 64:8. Kitia-moyo cha Maandiko kinachotolewa na programu hii kitatusaidia tufurahie zaidi hekima, haki, nguvu na upendo wa Yehova akiwa Mfinyanzi Mkuu.
Hotuba ya mwangalizi wa mzunguko yenye kichwa: “Kutumika Kama Vyombo Vyenye Kuheshimika Katika Kazi ya Kuhubiri,” itaonyesha jinsi watu wengi zaidi na zaidi wanavyoendelea kupata baraka kubwa ya kujua kweli na kuilezea watu wengine. Hotuba yenye kichwa: “Kufikiri Sana Juu ya Mambo Unayojifunza Kutakulinda,” itaonyesha jinsi ya kutafakari (kufikiri sana) kuhusu kanuni za Yehova za haki kunavyotulinda. Msemaji mgeni atatolea wasikilizaji hotuba yenye kichwa “‘Msifanyizwe Kulingana na Ulimwengu Huu’” na “Ujiache Kufinyangwa na Mfinyanzi Mkuu.” Wazazi na vijana watatiwa moyo na sehemu zenye kusema “Vijana Walio wa Mafaa kwa Yehova” na “Daraka la Maana la Wazazi Katika Tendo la Kufinyanga.” Kupitia maonyesho na sehemu za kuuliza watu maulizo, tutafurahi kusikia na kuona yale ambayo ndugu na dada zetu wanatimiza katika kazi ya kuhubiri. Wale wanaotaka kuonyesha wakfu wao kwa Mungu kwa kubatizwa katika maji wanapaswa kujulisha mwangalizi msimamizi wa kutaniko lao mbele ya wakati. Usisahau kuleta gazeti lako la Mnara wa Mlinzi la funzo litakalochunguzwa juma hilo la mkusanyiko wa pekee wa siku moja.
Mfinyanzi Mkuu anatimiza jambo lolote ambalo anakusudia. Lakini kila mmoja wetu anapaswa kujichagulia ikiwa atakubali kufinyangwa na Mfinyanzi Mkuu au hapana. Wale ambao kwa hekima wanatii kanuni na marekebisho ya Yehova wanaweza kurekebishwa, kutengenezwa na pia kufanywa kuwa vyombo vyenye mafaa, kama vile sehemu fulani ya udongo katika chombo cha kusagia udongo cha mfinyanzi. Tunapomuunga Yehova mkono, tunatukuza enzi yake kuu na kupata baraka nyingi.