Programu Mpya ya Mkusanyiko wa Pekee wa Siku Moja
Kichwa cha mkusanyiko wa pekee wa siku moja kwa ajili ya mwaka wa utumishi wa 2009 ni “Endelea Kuangalia Huduma . . . , Ili Uitimize.” Kichwa hicho kinategemea andiko la Wakolosai 4:17. Tukiwa Wakristo, tunachukua kwa uzito shauri hilo. Mradi wetu ni kutimiza kazi yetu ya kuhubiri kwa uaminifu, kama Yesu alivyofanya. (Yoh. 17:14) Mtume Paulo pia alikuwa mfano mzuri sana kwetu kuhusiana na jambo hilo. Alikusudia kabisa kumaliza mwendo wake katika kazi yake ya kuhubiri.—Mdo. 20:24.
Sehemu ya mwangalizi wa mzunguko itatuonyesha jinsi wahubiri mbalimbali wanashinda matatizo mengi katika mahubiri. Kisha hotuba yenye kichwa “Komaza Kile Ambacho Umepanda” itazungumzia jinsi gani tunaweza kuwasaidia kwa njia ya kweli wale walio na “mwelekeo unaofaa kwa ajili ya uzima wa milele.” (Mdo. 13:48) Msemaji mgeni atazungumzia kwanza andiko la 2 Wakorintho 6:1-10, mstari kwa mstari katika hotuba yenye kichwa “Jinsi Tunavyojipendekeza Wenyewe Kama Watumishi.” Kisha mchana-kati, atatoa hotuba yenye kichwa “Ona Kazi Yako ya Kuhubiri Kuwa ya Maana Sana.” Bila shaka, utapata kitia-moyo kutokana na hotuba “Vijana na Wazee Wanafurahia Kazi ya Kuhubiri” na “Vijana Wanaotimiza Kazi ya Kuhubiri.” Wale wanaotaka kuonyesha wakfu wao kwa kubatizwa kwenye mkusanyiko wa mzunguko ao wa pekee unaokuja, wanapaswa kumjulisha mwangalizi msimamizi mapema zaidi iwezekanavyo. Sehemu ya maana ya mikusanyiko yetu yote ni kifupi cha Mnara wa Mlinzi. Leta gazeti lako litakalochunguzwa katika juma la mkusanyiko wa pekee.
Tunapokuwa waangalifu kwamba tunatimiza kazi yetu ya kuhubiri, tunajikaza kuhakikisha kwamba mambo mengine na utendaji mbalimbali havituzuie kutimiza mgawo ambao Yehova ametutolea. Habari zenye kutia moyo kutoka katika maandiko zitakazotolewa kwenye mkusanyiko huu wa pekee wa siku moja, zitatusaidia sisi wote kuelewa yale ambayo tunahitaji kufanya ili kuendelea kuwa waangalifu na kufikiri juu ya mambo tunayofanya katika kazi ya kuhubiri ili kuitimiza vizuri kabisa.