Namna Gani Tutasaidia Wale Watakaohuzuria Ukumbusho?
1 Mwezi wa 3 tarehe 22, 2008, mamilioni ya watu ulimwenguni pote watapata ushahidi wenye nguvu. Wale watakaohuzuria Ukumbusho watasikia habari kuhusu upendo mwingi wa Yehova uliomchochea kutoa fidia kwa ajili ya wanadamu. (Yoh. 3:16) Watajifunza kuhusu Ufalme na jinsi Yehova atakavyoutumia ili kutimiza mapenzi yake duniani pote. (Mt. 6:9, 10) Watajionea upendo na umoja wa watu wa Mungu na jinsi tunavyokaribishana kwa uchangamfu.—Zab. 133:1.
2 Wanafunzi wa Biblia: Kati ya wasikilizaji, kutakuwa wale ambao wameanza kujifunza Biblia nasi hivi karibuni. Uwajulishe kwa ndugu na dada. Uwaeleze kuhusu mikutano ya kila juma, na kuwatolea maelezo mafupi kuhusu Jumba la Ufalme. Katika hotuba, msemaji atawatia moyo watu hao waendelee kufanya maendeleo ya kiroho. Unaweza kutumia maelezo yake ili kuwatia moyo wanafunzi wako wa Biblia.
3 Wahubiri Ambao Wameacha Kutenda: Kati ya wasikilizaji, kutakuwa pia wahubiri ambao wameacha kutenda. Ujikaze kuwasalimu kwa uchangamfu. Epuka kuwauliza maulizo kuhusu maisha yao ao kusema mambo yanayoweza kufanya wasikie haya. Muda mfupi kisha Ukumbusho, wazee watatembelea wale wote ambao wameacha kutenda waliohuzuria Ukumbusho, watawashukuru kwa kuwa wamejikaza kuhuzuria Ukumbusho na kuwaalika kwenye mkutano wa kutaniko unaofuata.
4 Wageni: Wengine kati ya wahuzuriaji wanaweza kuwa watu tunaofahamiana nao ao washiriki wa familia ambao sisi wenyewe tulialika. Labda wengine wamepokea kikaratasi cha mwaliko wakati wa kampanye ya pekee. Ukiona watu ambao haujui, ujijulishe kwao na kuwakaribisha. Labda hawajapata kuhuzuria hata mkutano wetu mmoja. Unapozungumza nao, unaweza kujua adresi yao na jinsi ya kupashana nao habari. Kwa kuwatembelea wewe mwenyewe ao kuzungumza nao kwa kifupi kwa njia ya telefone siku chache kisha Ukumbusho, unaweza kuwachochea wapendezwe zaidi na kuwauliza ikiwa watapenda kujifunza Biblia.
5 Tunapomtembelea mtu, tunaweza kutumia habari iliyozungumziwa katika hotuba ya Ukumbusho ili kumwonyesha kitabu Biblia Inafundisha. Kwa mfano, msemaji wa hotuba ya Ukumbusho atasoma Isaya 65:21-23. Unapomrudilia mtu, unaweza kutaja mambo fulani ya hotuba hiyo na kusema hivi: “Acha nikuonyeshe baraka zingine tunazoweza kupata kupitia fidia.” Kisha muchunguze ukurasa wa 4-5 wa kitabu Biblia Inafundisha. Ao unaweza kusema hivi: “Watu wengi wanajiuliza ni wakati gani tutaona kutimizwa kwa unabii wa Isaya.” Kisha muchunguze fungu la 1-3 katika sura ya 9. Namna ingine ni kutaja maelezo ya msemaji wa hotuba ya Ukumbusho, kuonyesha kitabu Biblia Inafundisha na kuonyesha jinsi funzo linavyofanywa.
6 Kila mmoja wetu na atafute nafasi za kusaidia wanafunzi wa Biblia, wahubiri ambao wameacha kutenda na wageni ambao watakuwa kwenye Ukumbusho. (Luka 22:19) Bila shaka, Yehova atatubariki tunapoongeza utendaji wetu katika utumishi wa Ufalme.
[Maulizo ya Funzo]
1. Ni ushahidi gani wenye nguvu utakaotolewa mwezi wa 3 tarehe 22, 2008?
2. Namna gani tutasaidia wanafunzi wa Biblia ambao watahuzuria Ukumbusho?
3. Namna gani tunaweza kutia moyo wahubiri ambao wameacha kutenda watakaohuzuria Ukumbusho?
4. Namna gani kila mmoja wetu anaweza kusaidia wageni?
5. Tunaweza kusema nini ili kuanzisha funzo la Biblia?
6. Ni nafasi gani tunazo tunapotii amri ya Yesu ya kuazimisha kifo chake?