Ushahidi Mkubwa Utatolewa
1. Zaidi ya hotuba, ni mambo gani mengine yanayoweza kuwavutia wageni kwenye Ukumbusho? Eleza.
1 Wakati gani? Mangaribi ya siku ya Ukumbusho. Tumejikaza kuwaalika watu waje wahuzurie Ukumbusho pamoja nasi. Wageni wanaohuzuria Ukumbusho hawavutiwi tu na yale wanayosikia. Kisha kuhuzuzia Ukumbusho, mwanamuke mmoja alitoa maelezo kuhusu yale aliyoona—hali ya urafiki ya kila mutu na jumba nzuri na safi lililojengwa na kutunzwa na watu wenye kujitolea. Kwa hiyo, sisi wote, si msemaji tu, tunatolea watu ushahidi kwenye tukio hilo la maana sana katika mwaka.—Efe. 4:16.
2. Namna gani kila mmoja wetu anaweza kutolea wageni ushahidi?
2 Salimu Wageni kwa Uchangamfu: Kuwaonyesha wageni sura ya kicheko na kuwasalimu kwa uchangamfu kutawatolea ushahidi. (Yoh. 13:35) Hata ikiwa hauwezi kuzungumza na kila mutu, unaweza kusalimu kwa uchangamfu watu watakaokaa karibu yako na kuwajulisha jina lako. (Ebr. 13:1, 2) Uwe mwangalifu ili kutambua wageni ambao wanaonekana kuwa hawafahamiane na mutu yeyote. Labda walipewa mwaliko wakati wa kampanye. Unaweza kuuliza, “Hii ndiyo mara yako ya kwanza kufika hapa?” Uwaombe wakae pamoja nawe, na uwe tayari kujibu maulizo yote wanayoweza kuuliza. Ikiwa kutaniko lenu linapaswa kuondoka haraka ili kuachia kutaniko lingine nafasi, unaweza kusema: “Ningependa kujua maoni yako kuhusu namna mambo yamepita. Namna gani tunaweza kuonana tena?”
3. Namna gani tunaweza kuwakaribisha wahubiri wasiotenda?
3 Karibisha Wahubiri Wasiotenda: Kwa kweli, wahubiri wasiotenda watafika kwenye Ukumbusho, kutia ndani wale ambao wanahuzuria tu Ukumbusho kila mwaka. Uwakaribishe, na uwajulishe kwamba unafurahi kabisa kuwaona. (Rom. 15:7) Muda mfupi baada ya Ukumbusho, wazee wanaweza kuwatembelea nyumbani kwao ili kuwatia moyo waendelee kushirikiana na kutaniko. Tunasali kwamba wengi kati ya wale watakaohuzuria Ukumbusho wachochewe kumtukuza Mungu, si kwa sababu tu ya mambo watakayosikia, lakini pia kwa sababu ya yale watakayoona ‘likiwa tokeo la matendo yetu mazuri ambayo wameshuhudia kwa macho.’—1 Pet. 2:12.