Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 11/08 uku. 4
  • Unaweza Kuwa Mwalimu!

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Unaweza Kuwa Mwalimu!
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Wahubiri wa Ufalme Wanapewa Mazoezi
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
  • Yehova Anatupatia Mazoezi ili Tufanye Kazi Hii
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Wazee, Munaona Namna Gani Kazi ya Kuzoeza Wengine?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Usijizuie Kuanzisha Funzo kwa Sababu Unawaza Hauna Uwezo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2008
km 11/08 uku. 4

Unaweza Kuwa Mwalimu!

1 Kufundisha mutu kweli ni moja kati ya sehemu zenye kupendeza zaidi za kazi yetu ya kuhubiri. Ni jambo la kufurahisha sana tunapomwona mutu huyo anakubali ujumbe wa Ufalme na tunapomsaidia amkaribie Mwenye Enzi Kuu ya ulimwengu wote mzima. (Yak. 4:8) Kusudi la kila mhubiri wa Ufalme linapaswa kuwa kumfundisha mutu ambaye ana njaa ya kujua kweli na kumwona mutu huyo akianza kufanya mabadiliko ya maana katika tabia, maoni, na mwenendo wake.—Mt. 28:19, 20.

2 Mtegemee Yehova: Wakati wa zamani, watumishi waaminifu walijisikia kwamba hawastahili kutimiza mgawo ambao Yehova aliwatolea. Kumtegemea Yehova kulimsaidia Musa, Yeremia, Amosi, na kulisaidia watu wengine wa maisha ya kawaida kuondoa mashaka ao wasiwasi yao, na walifikia kutimiza kazi ya maana. (Kut. 4:10-12; Yer. 1:6, 7; Amo. 7:14, 15) Mtume Paulo pia ‘alijipa ujasiri’ wa kusema. Jinsi gani? Alisema kwamba alifikia kufanya hivyo “kwa njia ya Mungu wetu.” (1 The. 2:2) Hakika, sisi wote tunaweza kumtegemea Yehova ili atutolee msaada, hekima, na nguvu tunayohitaji ili kuongoza mafunzo ya Biblia yenye kufanya maendeleo.—Isa. 41:10; 1 Kor. 1:26, 27; 1 Pet. 4:11.

3 Kubali Mazoezi: Mfundishaji wetu Mkuu, Yehova Mungu, anatutolea mazoezi kupitia programu ya kawaida ya mafundisho ya kiroho ili tuwe walimu wenye kustahili. (Isa. 54:13; 2 Tim. 3:16, 17) Kubali mazoezi hayo kwa kufaidika kabisa na kila mpango unaokupa nafasi ya kuongeza uelewaji wako wa Maandiko na kufanya uwezo wako wa kufundisha kweli za Biblia uwe mzuri zaidi. Hilo ndilo kusudi la kwanza la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi na Mkutano wa Utumishi. Mikutano mingine pia, yaani mikutano yote ya kutaniko inatuzoeza kufundisha Neno la Mungu.

4 Jikaze kujifunza njia rahisi za kufundisha hata kweli nzito za Biblia. Kitabu Shule ya Huduma, kwenye ukurasa wa 227, kinaeleza hivi: “ni lazima uelewe vizuri jambo unalozungumzia ikiwa utawasaidia wengine walielewe.” Kutoa maelezo kwenye mikutano kunatusaidia tuchunge akilini mambo ya maana ambayo tunaweza kutumia wakati ujao. Kwa hivyo, jitayarishe vizuri ili uwe na uhakika zaidi katika uwezo wako wa kufundisha.

5 Bila shaka, kuanzia mwanzo wahubiri Wakristo walijifunza kila mmoja kutoka kwa mwenzake walipokuwa wakitumika pamoja katika kazi ya kufanya wanafunzi. (Luka 10:1) Ikiwezekana, jiunge na wahubiri wanaozoea kazi ya kuhubiri, kama vile mapainia, wazee, na waangalizi wasafiri katika kazi ya kuongoza mafunzo ya Biblia. Angalia vizuri jinsi wanavyotumia mifano myepesi, na njia zingine za kufundisha zilizo katika vitabu vya funzo ili kufasiria kweli za Biblia. Uwaombe wakutolee mapendekezo yanayoweza kukusaidia kuwa mwalimu bora. (Met. 1:5; 27:17) Pendezwa na mazoezi yote hayo, kwa kuwa yanatolewa na Mungu.—2 Kor. 3:5.

6 Mtegemee Yehova, na faidika na mazoezi anayotoa. Katika sala, omba Yehova akusaidie kufanya maendeleo. (Zab. 25:4, 5) Wewe pia unaweza kupata furaha ya kumsaidia mutu kuwa mwalimu wa Neno la Mungu kama wewe.

[Maulizo ya Funzo]

1. Kila mhubiri wa Ufalme ana pendeleo gani la pekee?

2. Kwa nini wengine wanaweza kusita kuongoza funzo la Biblia, na ni nini kitakachowasaidia kushinda tatizo hilo?

3, 4. Ni programu gani zinazotuzoeza kufundisha Neno la Mungu?

5. Ni mazoezi mengine gani tunayopata katika kutaniko yanayotusaidia tuwe walimu wenye kufanya maendeleo?

6. Unahitaji kufanya nini ili uwe mwalimu wa Neno la Mungu?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine