Kisanduku Cha Maulizo
◼ Tunapaswa kufanya nini ikiwa tunaagizwa tuache kuhubiri mahali fulani?
Nyakati fulani, polisi wamewaendea wahubiri ambao walikuwa katika kazi ya kuhubiri, wakawaambia kwamba wanavunja sheria, na kuwaagiza waache kuhubiri. Ikiwa tunaagizwa tuache kuhubiri mahali fulani, tunapaswa kuondoka kwa heshima na bila kukawia. (Mt. 5:41; Flp. 4:5) Tusitafute kumaliza tatizo hilo sisi wenyewe kwa kuanzisha nao mabishano kuhusu haki zetu za kisheria. Ikiwezekana, tutafute kwa hekima namba ya kadi ya polisi huyo, na namba ya kituo cha polisi anapotumikia. Kisha, tuwajulishe wazee bila kukawia, nao pia watajulisha biro ya tawi kuhusu jambo hilo. Pia, ikiwa mkuu wa jengo fulani ao mutu mwingine anayesimamia jengo linalokaliwa na watu wengi anatuomba tuondoke, tutaondoka bila kuchelewa na kuwajulisha wazee. Tutaepuka matatizo yasiyo ya lazima ikiwa tunashugulika na wale wenye mamlaka kwa upole na kwa unyenyekevu.—Met. 15:1; Rom. 12:18.