Tafadhali Fanyeni Ziara Bila Kukawia
Kufanya ziara kwa nani? Kwa wale wanaoomba vichapo au kupelekewa magazeti kwa ukawaida au wale ambao wangetaka Shahidi awatembelee nyumbani kwao. Maombi hayo yanatoka wapi? Kwa watu wanaowasiliana na ofisi ya tawi kupitia barua au kwa njia ya simu au kupitia anwani yetu rasmi ya mtandao wa Internet. Kupendezwa kama huko kunapoonyeshwa, ofisi ya tawi itajulisha kutaniko la mahali kupitia fomu S-70, ambayo ni karatasi iliyo na kichwa “Veuillez à ce qu’un proclamateur expérimenté rende visite à cette personne.” Wazee wanapopokea fomu S-70, wanapaswa kuitoa mara moja kwa mhubiri atakayefuatia kwa bidii kupendezwa. Ikiwa ni vigumu kwa mhubiri kupata mtu huyo nyumbani, anaweza kujaribu kuwasiliana naye kwa njia ya simu au kutumia busara ili kumwachia barua ndogo. Ikiwa unaombwa kufanya ziara kama hiyo, tafadhali jitahidi kuwasiliana na yule anayependezwa bila kukawia.