Tenda Bila Kukawia
Tangu adresi yetu mupya ya internete ilianza kutumika, watu wengi sana wameomba funzo la Biblia kupitia adresi hiyo. Njia mupya za kuhubiri mahali pa watu wengi zimeongeza pia ombi zingine za mafunzo. Biro ya tawi inashugulikia haraka ombi hizo mara tu inapozipata. Kwa mufano, kila mara mutu fulani akiomba funzo kupitia adresi yetu jw.org, biro ya tawi inawajulisha wazee wa kutaniko la eneo la mutu huyo siku mbili tu baadaye. Lakini, ripoti zinaonyesha kwamba watu fulani ambao wameomba funzo la Biblia hawakutembelewa mbele ya majuma fulani. Namna gani tunaweza kuhakikisha kwamba mutu huyo anatembelewa wakati angali anapendezwa?—Mk. 4:14, 15.
Ikiwa mutu fulani ambaye haishi katika eneo lenu anapendezwa, jaza bila kukawia fomu Tafadhali Fuatia Upendezi (S-43) na uipatie mwandishi wa kutaniko lenu siku ya mikutano inayofuata ao mbele ya hapo. Kisha, mwandishi wa Kutaniko atatuma fomu hiyo katika kutaniko la eneo la mutu huyo ao kwenye biro ya tawi katika muda wa siku moja ao mbili kwa kutumia adresi ya kutaniko kwenye jw.org. Wazee wa kutaniko wanapaswa kufungua adresi hiyo ya kutaniko kila mara. Ikiwa wanapata habari ya kumutembelea mutu fulani, wanapaswa kutenda bila kukawia. Muhubiri yeyote atakayeombwa kutembelea mutu huyo, anapaswa kumuona haraka. Ikiwa haupate mutu huyo nyumbani mwake, pengine unaweza kuacha barua fulani iliyo na adresi yako yote.