Uwe Tayari Kuanzisha Funzo la Biblia
1. Ni jambo gani tunalopaswa kufanya ili kutimiza kazi ambayo Yesu alituachia kulingana na Mathayo 28:19, 20?
1 Yesu alituachia kazi ya ‘kufanya wanafunzi na kuwafundisha.’ (Mt. 28:19, 20) Kwa hiyo, tunapenda kuwa tayari kuanzisha funzo la Biblia kila nafasi inapojitokeza wala si kufanya hivyo tu siku iliyopangwa kwa ajili ya kuanzisha mafunzo ya Biblia. Mapendekezo yanayofuata yanaweza kutusaidia.
2. Ni nani tunaweza kutolea funzo la Biblia?
2 Tolea Watu Funzo: Kadiri tunavyotolea watu Funzo la Biblia, ndivyo tunavyopata nafasi zaidi ili kupata mafunzo. (Mhu. 11:6) Je, Umejaribu kuanzisha funzo la Biblia moja kwa moja? Kutaniko moja katika Amerika lilijikaza kufanya hivyo mwezi mzima. Walifurahi sana kuanzisha mafunzo mapya ya Biblia 42! Usiwazie tu kwamba wale wanaopendezwa wanajua kwamba wewe unafundisha watu Biblia. Unapowarudilia tena, kwa nini usiwatolee funzo la Biblia? Ikiwa hawakubali funzo la Biblia kwa wakati huo, hakuna shida. Unaweza kuendelea kuwasaidia wapendezwe. Je, umeuliza majirani wako, watu wa jamaa, wafanyakazi wenzako, na wanafunzi wenzako ikiwa wanapenda kujifunza Biblia pamoja nawe? Unaweza pia kuuliza wale unaojifunza nao Biblia ikiwa wana marafiki ao watu wa jamaa zao ambao wanapenda kujifunza Biblia.
3. Ni chombo gani kinachoweza kutusaidia kuanzisha mafunzo, na ni wakati gani tunaweza kukitumia?
3 Chombo Chenye Kusaidia: Chombo cha maana sana kinachoweza kutusaidia ili kuanzisha mafunzo ya Biblia ni trakti Je, Ungependa Kujua Kweli? Unaweza kuwatolea wasikilizaji trakti hiyo hata ikiwa wanakubali vitabu vingine ao hapana. Tunaweza kutumia trakti hiyo tunapohubiri mahali pa biashara, barabarani, tunapotumia watu barua, na tunaporudilia wale waliopendezwa. Tunaweza pia kuiacha mahali ambapo hatukukuta watu nyumbani. Kwa nini usiichukue unapochukua taksi, unapokwenda kununua vitu kwenye maduka ao sokoni, na unapokwenda kazini? Ukurasa wa mwisho wa trakti hiyo unaeleza kwa kifupi mpango wa funzo la Biblia kupitia kitabu Biblia Inafundisha.
4. Namna gani tunaweza kutumia trakti Kujua Kweli ili kuanzisha funzo la Biblia?
4 Kisha kumtolea mutu trakti hiyo, unaweza kumuonyesha maulizo yaliyo kwenye ukurasa wa kwanza na kumuuliza, “Ni ulizo gani kati ya maulizo haya linalokupendeza?” Kisha muchunguze jibu kutoka katika trakti, na kusoma ao kutaja sehemu iliyo kwenye ukurasa wa mwisho, inayozungumzia mpango wa funzo la Biblia. Kisha unaweza kumuonyesha mahali, katika kitabu Biblia Inafundisha, ambako atapata maelezo zaidi kuhusu habari hiyo. Umutolee kitabu, na ufanye mipango ya kumurudilia ili kuendelea na mazungumzo.
5. Kwa nini tunapaswa kuwa tayari kuanzisha funzo la Biblia?
5 Eneo letu lingali na wale walio na hamu ya kujifunza yale ambayo Biblia inafundisha kabisa. Kwa kuwa tayari kuanzisha funzo la Biblia, tutapata furaha zaidi inayotokana na kusaidia wengine ili wapate njia ya uzima.—Mt. 7:13, 14.