Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 01/12/10
“Je, unakubali kwamba mara nyingi wazazi wanaowalea watoto peke yao wanapata magumu mengi kupita wazazi walio na wenzi? [Acha mutu ajibu.] Biblia inatutia moyo tutende kwa kuwafikiria wale walio na magumu. [Soma Zaburi 41:1.] Habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 22 inaeleza jinsi tunavyoweza kuwafikiria wazazi wanaowalea watoto peke yao.”
Amkeni! Mwezi wa 12
“Watu wengi wamejiuliza, ‘Ikiwa Mungu yuko, kwa nini hamuharibu Ibilisi?’ Je, umekwisha kujiuliza hivyo? [Acha mutu ajibu.] Habari iliyo kwenye ukurasa wa 10 na wa 11 inatoa maoni ya Biblia kuhusu ulizo hilo. Inatuelezea pia jinsi ulimwengu utakavyokuwa wakati Ibilisi hatakuwapo tena.” Soma Ufunuo 21:3, 4.
Mnara wa Mlinzi 01/01/11
“Watu wengi wanaamini kwamba habari kuhusu shamba la Edeni si ya kweli. Je, utashangazwa kujua kwamba Yesu alionyesha kwamba Adamu na Hawa ni watu waliopata kuishi? [Acha mutu ajibu. Kisha soma Mathayo 19:4-6.] Gazeti hili linatoa majibu kwa maulizo ambayo watu wengi wanajiuliza kuhusu shamba la Edeni.”
Amkeni! Mwezi wa 1
Onyesha jalada na kisha uliza, “Wewe ungejibu ulizo hili namna gani? [Acha mutu ajibu.] Maandiko yanatutia moyo tufanye amani na watu wote. [Soma Yakobo 3:17.] Kwa nini basi dini zimeshindwa kuunganisha watu? Je, dini zitawasaidia wanadamu wapate kuishi kwa amani? Gazeti hili linatoa majibu kwa maulizo hayo.”