Njia Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
Jinsi ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Siku ya Posho ya Kwanza Katika Mwezi wa 1
“Watu fulani wanaamini kwamba Biblia ni kitabu kilicho na unabii wenye kutegemeka. Wengine wanafikiri kwamba inatabiri mambo yasiyoeleweka waziwazi ambayo watu wanaweza kufasiria kwa njia mbalimbali, kulingana na maoni yao. Wewe unafikiri nini?” Acha mutu ajibu. Umuonyeshe mutu Mnara wa Mlinzi wa tarehe 1 mwezi wa 1, na musome na kuzungumuzia habari ya kichwa kidogo cha kwanza kwenye ukurasa wa 16 na andiko moja hivi kati ya maandiko yanayoonyeshwa. Umutolee mutu magazeti, na ufanye mupango wa kumurudilia ili kuzungumuzia ulizo linalofuata.
Mnara wa Mlinzi 01/01/12
“Tunaweza kujifunza mambo mengi kutokana na wanaume na wanawake wanaojulikana sana katika historia, sivyo? [Acha mutu ajibu.] Andiko hili la Biblia linazungumuzia mutu mumoja anayejulikana sana, ni yeye tu ndiye Biblia inaita ‘rafiki ya Mungu.’ [Soma Yakobo 2:23.] Gazeti hili linaonyesha kwa nini Abrahamu alikuwa rafiki ya Mungu na linazungumuzia yale tunayoweza kujifunza kutokana na mufano wake.”
Amkeni! Mwezi wa 1
“Kutoa rushwa, kukata midomo, na namna zingine za wizi na uongo ni mambo yanayofanywa na watu wengi katika mambo ya biashara. Watu fulani wanafikiri kwamba ni lazima kuiba na kusema uongo katika biashara ili kupata faida. Wewe unafikiri nini? [Acha mutu ajibu.] Ona maneno haya yanayoweza kumufanya mutu afikiri. [Soma Methali 20:17.] Gazeti hili linaeleza kwa nini ni vizuri kuwa mwaminifu katika mambo yote.”