Namna Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
Namna ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Siku ya Posho ya Kwanza ya Mwezi wa 1
“Watu wengi wana mawazo yao juu ya Mungu. Wamoja wanawaza kama Mungu ni nguvu fulani isiyoeleweka. Wengine wanamuona Mungu kuwa Baba wa mbinguni mwenye upendo. Wewe unawaza nini?” Acha mutu ajibu. Umuonyeshe ukurasa wa mwisho wa Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 1, na muzungumuzie habari iliyo chini ya ulizo la kwanza na hata andiko moja. Umutolee magazeti, na upange kumurudilia ili kuzungumuzia ulizo linalofuata.
Munara wa Mulinzi 01/01
“Tunawatembelea watu ili kuzungumuza nao juu ya hali inayotuhuzunisha sisi wote, ni kusema kifo cha mutu fulani ambaye tunapenda. Hauone kwamba kifo cha rafiki ao mutu wa familia yako, ni moja kati ya hali ambazo ni vigumu kupambana nazo? [Acha mutu ajibu.] Andiko hili la Biblia limewafariji watu wengi. [Soma Isaya 25:8.] Gazeti hili linazungumuzia ahadi ya Biblia yenye kutia moyo, ni kusema, Mungu atamaliza kifo na atafufua watu tuliowapenda.”
Amuka! Mwezi wa 1
“Unakubali kwamba leo familia zinapambana na magumu mengi? [Acha mutu ajibu.] Mezali hii ya Biblia inatuonyesha mambo ambayo familia zinapaswa kufanya ili kupambana na magumu yao na kusaidia familia zao. [Soma Methali 24:3.] Watu wengi wametambua kwamba wanaweza kutegemea Biblia ili kupata hekima. Gazeti hili linazungumuzia adresi moja ya Internete inayotegemea Biblia. Ni adresi hiyo tu ndio ina habari fulani zinazosaidia familia bila kulipa.”