Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 3/12 uku. 3
  • Maajabu ya Uumbaji Yanafunua Utukufu wa Mungu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Maajabu ya Uumbaji Yanafunua Utukufu wa Mungu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Ujifunze Mambo Mingi Zaidi juu ya Yehova Kupitia Uumbaji
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
  • Unaona Sifa za Mungu Zenye Hazionekane?
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2019
  • Mufundishe Watoto Wenu juu ya Yehova Kupitia Uumbaji
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
  • Uumbaji Unaonyesha Upendo wa Yehova
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2021
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2012
km 3/12 uku. 3

Maajabu ya Uumbaji Yanafunua Utukufu wa Mungu

Watu wengi wanafurahia kutazama uumbaji ao vitu vilivyoumbwa. Lakini ni watu wachache tu ndio wanaotambua kama viumbe vinafunua mawazo na sifa za Muumbaji wetu Mukubwa. (Rom. 1:20) Wakati wa zamani, Daudi alijifunza juu ya Yehova kwa kusoma Neno Lake. Lakini pia “alimuona” Yehova na kumukaribia kwa kutazama vitu Yehova aliumba. (Zab. 8:3, 4) Video yenye kichwa Maajabu ya Uumbaji Yanafunua Utukufu wa Mungu inatusaidia kuchunguza kwa uangalifu viumbe fulani vya Yehova na kuona sifa za Muumbaji wetu Mukubwa. Inasaidia pia watoto wetu na watu tunaojifunza nao Biblia. Kuchunguza kwa uangalifu viumbe vya Yehova na kuona sifa zake kunatufanya tumukaribie zaidi. Basi, tazama video hiyo na kisha kuitazama, jaribu kujibu maulizo yanayofuata.

(1) Namna gani ukubwa wa ulimwengu na namna vitu vinatembea kwa utaratibu katika ulimwengu wote vinatusaidia kumuogopa Yehova zaidi? (Isa. 40:26) (2) Tunapochunguza maji kwa uangalifu, tunaweza kujifunza nini juu ya Muumbaji wa maji? (Ufu. 14:7) (3) Namna gani ukubwa wa dunia na umbali ulio kati ya dunia na jua vinaonyesha hekima ya Yehova? (4) Mwezi unafanya kazi gani? (Zab. 89:37) (5) Ni nini inayoonyesha kama Yehova alituumba ili tufurahie maisha? (6) ADN ni nini? (Zab. 139:16) (7) Namna gani watu ni tofauti sana na viumbe vingine vyote ambavyo Yehova aliumba duniani? (Mwa. 1:26) (8) Unangojea nini katika dunia mupya?

Sehemu za Ziada: (9) Rangi zinatokea namna gani? (10) Namna gani maji yanaingia katika muti na kupanda mupaka kwenye matawi ya muti? (11) Maji yanafanya kazi gani katika mwili wetu? (12) Toa mifano inayoonyesha namna viumbe vilivyo na uzima vinapatana. (13) Namna gani viumbe vinasaidiana? (14) “Pembe bora” ni nini, na namna gani inaonekana katika viumbe? (Soma Amkeni! ya mwezi wa 9, 2006, ukurasa wa 24, 25).

‘Muangalie kwa Uangalifu Viumbe vya Yehova: Yesu alitutia moyo tuangalie kwa makini ao kwa uangalifu ndege wa mbinguni na ‘tujifunze kwa mayungiyungi ya shamba.’ (Math. 6:26, 28) Kwa kufanya hivyo, imani yetu inaweza kuwa nguvu zaidi, tunaweza kumutegemea Muumbaji wetu, na tunaweza kuelewa zaidi hekima yake, uwezo wake wa kuokoa, na upendo wake. Kuliko kukengeushwa na mambo ya ulimwengu huu, tujipangie wakati wa kutazama maajabu ya uumbaji wa Yehova na tujikaze sana kufanya hivyo, na kisha tufikiri sana juu ya mambo ambayo viumbe vinatufundisha juu ya Mungu wetu.—Zab. 19:1.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine