Kisanduku Cha Maulizo
◼ Tunapohuzuria mikutano ya Kikristo na tunapokuwa katika mahubiri, ni kanuni gani za Biblia zinazoweza kutuongoza kuhusu matumizi ya telefone?
“Kuna Wakati Uliowekwa wa Kila Kitu.” (Mhu. 3:1): Telefone inawezesha watu kuzungumuza ao kutumiana ujumbe wakati wowote. Lakini, kuna nyakati ambazo Wakristo hawapende kukengeushwa na telefone. Kwa mufano, mikutano yetu ni wakati wa kumuabudu Yehova, kupokea mafundisho ya kiroho, na kutiana moyo. (Kum. 31:12; Zab. 22:22; Rom. 1:11, 12) Unaweza kuzima telefone yako unapofika kwenye mikutano na kusoma ujumbe wowote wanaokutumia kisha mikutano. Ikiwa unatazamia hali fulani inayoomba kutenda kwa uharaka, na kwa hiyo unalazimika kuacha telefone yako wazi, unapaswa kuiweka katika hali ambayo haitawasumbua wengine.
‘Fanya Mambo Yote kwa Ajili ya Habari Njema.’ (1 Kor. 9:23): Nyakati fulani, tunaweza kutumia telefone kwa njia inayofaa katika mahubiri. Kwa mufano, ndugu anayeongoza mukutano kwa ajili ya mahubiri anaweza kuitumia ili kuzungumuza na wale wanaohubiri katika sehemu zingine za eneo. Wakati fulani wahubiri wanatumia telefone ili kuita mutu anayependezwa ao mwanafunzi wa Biblia mbele ya kumutembelea, zaidi sana ikiwa mutu huyo anaishi mbali. Ikiwa tuna telefone, tunapaswa kuchukua mipango ili isikatize mazungumuzo yetu na musikilizaji. (2 Kor. 6:3) Unapongojea wahubiri wenzako, kuliko kuitaita marafiki ao kuwatumia ujumbe, inaweza kuwa jambo nzuri kukazia uangalifu mahubiri na wale unaohubiri nao.
Uwafikirie Wengine. (1 Kor. 10:24; Flp. 2:4): Tusichelewe mikutano kwa ajili ya mahubiri kimakusudi tukifikiri kwamba hata ikiwa tunachelewa, tunaweza kumuita ndugu anayeongoza ao kumutumia muhubiri fulani ujumbe ili kujua mahali ambapo kikundi kinahubiri. Tunapochelewa, kwa kawaida ndugu anayeongoza mukutano kwa ajili ya mahubiri analazimika kuwapanga tena watu. Bila shaka, hali zisizotazamiwa zinaweza kufanya wakati fulani tuchelewe. Hata hivyo, ikiwa kila mara tunafika pa wakati, tunaonyesha kwamba tunaheshimu mupango wa Yehova, tunafikiria ndugu anayeongoza mukutano, na wahubiri wenzetu.