Namna Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
Namna ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Siku ya Posho ya Kwanza Katika Mwezi wa 5
“Sisi wote tunafanya makosa. Je, umekwisha kujiuliza ikiwa Mungu anaweza kusamehe hata matendo mabaya sana?” [Acha mutu ajibu.] Umuonyeshe habari iliyo kwenye ukurasa wa 15 wa Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 5, na muzungumuzie habari iliyo chini ya ulizo la kwanza na hata andiko moja. Umutolee magazeti, na upange kumurudilia ili kuzungumuzia ulizo linalofuata.
Munara wa Mulinzi 01/05/13
“Tungependa kujua maoni yako juu ya andiko hili. [Soma 1 Yohana 4:8.] Watu wengi wanakubali kwamba Mungu ni upendo, lakini wengine wanawaza kama Mungu hana huruma kwa sababu anasababisha misiba, ao anaiacha itupate. Wewe unawaza nini? [Acha mutu ajibu.] Gazeti hili linaeleza sababu gani hatupaswe kufikiri kwamba Mungu hana huruma.”
Amkeni! Mwezi wa 5
“Tunawatembelea majirani wetu ili kuzungumuza nao kuhusu uovu, tatizo linalohangaisha sana watu. Watu fulani wanawaza kama siri ya kumaliza uovu ni kuongeza mapolisi. Wewe unawaza nini? [Acha mutu ajibu.] Je, unajua kwamba Biblia imeahidi kama uovu utakwisha? [Soma Zaburi 37:10, 11.] Gazeti hili linazungumuzia jambo hilo na linatuonyesha mambo fulani ambayo tunaweza kufanya ili kujilinda na uovu.”