Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 4/14 uku. 6-7
  • Trakte Mupya Zenye kuvutia Sana!

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Trakte Mupya Zenye kuvutia Sana!
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tumia Trakte ili Kueneza Habari Njema
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Namna ya Kuanzisha Mazungumuzo kwa Kutumia Trakte
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2020
  • Neno la Mungu Liko Hai!—Ulitumie
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Tumieni trakti ili kuanzisha mazungumzo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2014
km 4/14 uku. 6-7

Trakte Mupya Zenye kuvutia Sana!

1. Tumepata vyombo gani vyenye kuvutia sana kwa ajili ya mahubiri?

1 Trakte mupya tano zilitolewa kwenye Mukusanyiko wa Wilaya wa 2013 wenye kichwa “Neno la Mungu Ni Kweli!” Pia, trakte Habari ya Ufalme Na. 38, yenye kichwa “Watu Waliokufa, Wanaweza Kweli Kuishi Tena?” iliongezwa. Trakte hizo 6 ni zenye kuvutia sana. Sababu gani trakte hizo zimekuwa na ukubwa na umbo mupya? Tunapohubiri nyumba kwa nyumba, namna gani tunaweza kuzitumia?

2. Trakte zetu mupya zina kusudi gani?

2 Sababu Gani Zina Umbo Mupya?: Kwa kawaida, ili kupata matokeo mazuri katika mahubiri ya nyumba kwa nyumba, ni muzuri kufuata hatua ine: (1) Kumuuliza mwenye​-nyumba ulizo linalomufanya atoe maoni yake ili kuanzisha mazungumuzo. (2) Kumuonyesha yale ambayo Biblia inasema. (3) Kumuachia kichapo. (4) Kutokeza ulizo mbele ya kuachana naye, na kufanya mipango ya kumurudilia ili kujibia ulizo hilo. Trakte hizo mupya zinatusaidia kufuata hatua hizo ine bila magumu.

3. Tunapohubiri, namna gani tunaweza kuwaachia watu trakte mupya?

3 Namna ya Kuzitumia: (1) Kisha kumusalimia mutu, umuonyeshe ulizo lililo kwenye ukurasa wa kwanza, kisha umuombe achague jibu hapo chini. (2) Fungua trakte, na muchunguze sehemu “Ona Jibu la Biblia.” Ikiwa hali zinaruhusu, soma moja kwa moja andiko lililo hapo katika Biblia. Ikiwa musikilizaji ana wakati, muzungumuzie sehemu “Utapata Faida Gani Ukiamini Fundisho Hilo la Biblia?” (3) Umuachie trakte, na umutie moyo aisome. (4) Mbele ya kuondoka, umuonyeshe ulizo lililo kwenye ukurasa wa mwisho, chini ya kichwa “Ukitaka Kujua Mengi” na ufanye mipango ya kumurudilia ili kuona jibu la Biblia.

4. Namna gani tunaweza kutumia trakte mupya wakati tunamurudilia mutu?

4 Ni rahisi pia kuwarudilia watu. Tumia tu maandiko yanayoonyeshwa kwenye ukurasa wa mwisho ili kujibia ulizo ulilotokeza mwishoni mwa mazungumuzo yenu ya kwanza. Mbele ya kuondoka, onyesha musikilizaji picha ya broshua Habari Njema kwenye trakte, umuonyeshe broshua yenyewe na somo lililo na habari zaidi kuhusu mambo munayozungumuzia, kisha umuachie broshua hiyo. Akiikubali, fanya mipango ya kumurudilia ili muzungumuzie broshua hiyo. Ukifuata hatua hizo, utakuwa umeanzisha funzo la Biblia! Ao, kuliko kumuachia broshua, unaweza kumuachia trakte ingine na kufanya mipango ya kumurudilia ili kuzungumuzia trakte hiyo.

5. Trakte zinatimiza kazi gani katika mahubiri?

5 Tumetumia trakte katika mahubiri kwa miaka zaidi ya 130. Hata kama zimebadilika kwa ukubwa na umbo, trakte ni vifaa ambavyo vimekuwa na matokeo mazuri katika mahubiri. Basi, na tutumie vizuri vifaa hivyo vipya vyenye kuvutia sana ili kueneza ujuzi wa Biblia duniani pote.​—Met. 15:7a.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine