MAISHA YA MUKRISTO
Namna ya Kuanzisha Mazungumuzo kwa Kutumia Trakte
Tangu Mwezi wa 1, 2018, ukurasa wa kwanza wa Buku la Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo umekuwa na namna mbalimbali za kuanzisha mazungumuzo. Tumetiwa moyo kuzungumuza zaidi na watu kuliko tu kuwapatia vichapo. Juu ya kusaidia wahubiri kufanya vile, video mbalimbali za namna ya kuanzisha mazungumuzo zimeonyesha namna ya kuanzisha mazungumuzo kwa kutumia tu Biblia. Lakini, ni kusema kama hatupaswe tena kutumia vichapo wakati tuko tunahubiri nyumba kwa nyumba? Haiko vile! Kwa mufano, tunaweza kupata matokeo ya muzuri kwa kuanzisha mazungumuzo kupitia trakte. Tunaweza kutumia ufundi wenye kufuata wakati tuko tunatumia trakte yoyote kati ya trakte zetu:
Uliza mutu ulizo lenye kuwa ku ukurasa wa kwanza, kisha umuombe achague jibu moja kati ya majibu mbalimbali yenye kuonyeshwa.
Onyesha jibu la Biblia kwa kutumia andiko ao maandiko yenye kuwa ku mwanzo wa ukurasa wa pili. Kama kungali wakati, soma na muzungumuzie habari fulani yenye kuwa ndani ya ile trakte.
Umupatie musikilizaji trakte, kisha umutie moyo asome mambo ingine yenye kuwa ndani.
Mbele uachane naye, umuonyeshe sehemu “Fikiria Ulizo Hili” na umuambie kama utamurudilia wakati mwingine ili kuzungumuzia jibu la Biblia.
Wakati unamurudilia, muzungumuzie jibu kisha umuachie ulizo lenye mutazungumuzia wakati mwingine. Unaweza kuchagua ulizo moja ku site yetu ya Enternete ao mu kichapo chenye kinaonyeshwa kwenye ukurasa wa mwisho. Kwa wakati wenye kufaa, umutolee broshua Habari Njema Yenye Inatoka kwa Mungu! ao kichapo kingine cha funzo chenye kuwa kati ya Vyombo Vyetu vya Kufundishia.