Tumia Trakte ili Kueneza Habari Njema
1. Watu wa Mungu wamezitumia trakte namna gani?
1 Tangu zamani watu wa Mungu wametumia trakte zinazotegemea Biblia ili kueneza habari njema. Katika mwaka wa 1880, ndugu Russell na wafanyakazi wenzake walianza kutokeza Bible Students’ Tracts, (Trakte za Wanafunzi wa Biblia) na trakte hizo zilitolewa kwa wasomaji wa Munara wa Mulinzi ili wazigawanyie watu. Trakte zilionwa kuwa za lazima sana hivi kwamba katika mwaka wa 1884 ndugu Russell alipoandikisha kisheria shirika lisilotafuta faida ili kuendeleza kazi ya Ufalme, neno “trakte” lilitiwa katika jina, Zion’s Watch Tower Tract Society; leo inaitwa Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania. Kufikia mwaka wa 1918, wanafunzi wa Biblia walikuwa wamegawanya trakte zaidi ya milioni 300. Hata leo, trakte zinaendelea kutumiwa na zina matokeo mazuri katika mahubiri.
2. Sababu gani trakte zina matokeo mazuri?
2 Sababu Gani Zina Matokeo Mazuri: Trakte zina picha nzuri na zinavutia. Ujumbe mufupi ulio ndani ni wenye kuvutia na unafundisha kabisa. Zinawapendeza wasikilizaji ambao wanaweza kusita kuchukua gazeti ao kitabu. Ni rahisi kutolea watu trakte; hata wahubiri wapya na watoto wanaweza kuzitolea watu. Tena, trakte si kubwa na ni rahisi kuzibeba.
3. Eleza jambo ulilojionea ao ulilosoma katika vichapo linaloonyesha kama trakte zina matokeo mazuri.
3 Watu wengi walijifunza kuhusu kweli kwa mara ya kwanza kupitia trakte. Kwa mufano, katika inchi ya Haiti mwanamuke mumoja aliona trakte yetu chini katika barabara. Aliiokota, akaisoma, na kusema, “nimeipata kweli!” Mwishowe, alienda kwenye Jumba la Ufalme, akaanza kujifunza Biblia, na akabatizwa—yote hayo kwa sababu ya nguvu ya Neno la Mungu iliyo katika trakte.
4. Kusudi letu ni gani wakati trakte ndizo toleo la mwezi?
4 Tunapohubiri Nyumba kwa Nyumba: Kwa kuwa trakte zina matokeo mazuri katika mahubiri, kuanzia Mwezi wa 11, mara kwa mara zitakuwa toleo la mwezi. Kusudi letu si kuwatolea tu watu trakte lakini ni kuitumia ili kuanzisha mazungumuzo. Ikiwa mutu unayehubiria kwa mara ya kwanza ao mutu unayerudilia anapendezwa, unaweza kumuonyesha namna tunavyojifunza Biblia pamoja na watu kwa kutumia kitabu Biblia Inafundisha ao kitabu kingine cha funzo. Namna gani tunaweza kumutolea mutu trakte tunapohubiri nyumba kwa nyumba? Kwa kuwa kila trakte ni tofauti na ingine, ni lazima tujue habari zilizo katika trakte tunazotolea watu.
5. Namna gani tunaweza kutolea watu trakte tunapohubiri nyumba kwa nyumba?
5 Utangulizi wetu utapatana na hali ya watu wa eneo letu na habari iliyo katika trakte tunayotumia. Tunaweza kuanzisha mazungumuzo kwa kumupatia musikilizaji trakte. Ukurasa wa kwanza ulio na picha zenye kuvutia unaweza kuamusha kupendezwa kwake. Ao tunaweza kumuonyesha trakte mbalimbali na kumuomba achague ile inayomupendeza. Tunapohubiri katika eneo ambamo watu wanasita kuwafungulia wageni milango yao, tunaweza kushika trakte kwa namna ya kwamba musikilizaji aone ukurasa wa kwanza, ao tunaweza kumuuliza ikiwa tunaweza kuiingiza chini ya mulango na kwamba tungependa kujua maoni yake juu ya trakte hiyo. Ikiwa kichwa cha trakte ni ulizo, tunaweza kumuomba atuelezee mawazo yake juu ya ulizo hilo. Ao tunaweza kutokeza ulizo ambalo linaweza kuamusha kupendezwa na kumuchochea kuzungumuza. Kisha tunaweza kusoma sehemu fulani katika trakte pamoja na musikilizaji. Mahali palipo ulizo, tutatua na kumuomba atoe mawazo yake. Maandiko ya musingi yanaweza kusomwa katika Biblia. Kisha kuzungumuzia habari fulani, tunaweza kumaliza mazungumuzo na kufanya mipango ya kumurudilia. Ikiwa kwa kawaida munaacha vichapo mahali ambapo hamuwakute watu, munaweza kuacha trakte, lakini ni vizuri kuhakikisha kwamba munaitia mahali ambapo wapitanjia hawataiona.
6. Namna gani tunaweza kutumia trakte tunapohubiri barabarani?
6 Tunapohubiri Barabarani: Je, umekwisha kutumia trakte unapohubiri barabarani? Wapitanjia fulani wako haraka na hawana nia ya kusimama ili kuzungumuza nasi. Inaweza kuwa vigumu kujua ikiwa watapendezwa ao hapana. Kuliko kuwapatia magazeti ya hivi karibuni bila kujua ikiwa watayasoma, ni vizuri zaidi kuwapatia trakte. Kwa sababu ukurasa wa kwanza wa trakte ni wenye kuvutia na ina habari fupi, hamu ya kutaka kujua inaweza kumuchochea mutu aisome anapopata wakati. Bila shaka, ikiwa mupitanjia hana haraka, tunaweza kuzungumuzia habari fulani iliyo katika trakte pamoja naye.
7. Eleza mambo yaliyoonwa yanayoonyesha namna ya kutumia trakte tunapohubiri wakati hatukupanga kufanya hivyo.
7 Tunapohubiri Wakati Hatukupanga Kufanya Hivyo: Ni rahisi kuhubiri wakati hatukupanga kufanya hivyo kwa kutumia trakte. Ndugu mumoja anaweka trakte fulani katika mufuko wa nguo yake kila mara anapoondoka nyumbani. Anapokutana na mutu, kwa mufano, mutu anayeuzisha ndani ya duka, anamuuliza kama anaweza kumupatia kitu cha kusoma, na kisha anamupatia trakte. Wakati ndugu mumoja na bibi yake walitembelea New York ili kujionea muji huo, walitambua kama wangeweza kukutana na watu kutoka inchi mbalimbali. Kwa hiyo, walienda na kijitabu Habari Njema kwa Watu wa Mataifa Yote na trakte katika luga mbalimbali. Hivyo, wakati walisikia mutu akisema luga ya kigeni, kwa mufano, mutu mwenye kuuzisha vitu pembeni ya barabara, ao mutu mwenye kukaa karibu nao katika bustani ao katika restora, walimutolea trakte katika luga yake.
8. Trakte zinaweza kufananishwa na mbegu katika njia gani?
8 “Panda Mbegu Zako”: Trakte zinaweza kufananishwa na mbegu. Mulimaji anapanda mbegu nyingi katika shamba lake kwa sababu hajue ni mbegu gani itakayoota na kuchipuka. Andiko la Mhubiri 11:6 linasema hivi: ‘Asubuhi panda mbegu zako na mupaka mangaribi usiache mukono wako upumuzike; kwa maana haujue ni wapi hii itafanikiwa, hapa ao pale, ao ikiwa zote mbili zitakuwa njema.’ Kwa hiyo, acheni basi ‘tutawanye ujuzi sikuzote’ kwa kutumia trakte tunapohubiri.—Met. 15:7.
[Wazo la fungu kwenye ukurasa 3]
Kwa kuwa trakte zina matokeo mazuri katika mahubiri, kuanzia Mwezi wa 11, mara kwa mara zitakuwa toleo la mwezi