Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri—Tayarisha Maneno Yako ya Utangulizi
Sababu Gani Ni Lazima Kufanya Hivyo: Ikiwa maneno yetu ya utangulizi hayapendeze, musikilizaji anaweza kukatiza mazungumuzo mbele sisi kumuhubiria. Kwa hiyo, wahubiri wengi wanaona kwamba maneno yao ya utangulizi ni ya maana sana ili kuanzisha mazungumuzo. Hata kama namna mbalimbali za kuanzisha mazungumuzo zinapatikana katika Huduma Yetu ya Ufalme na katika kitabu Kutoa Sababu, vichapo hivyo havitutolee kila mara maneno yote ya utangulizi; kwa hiyo, tuna nafasi ya kupatanisha mazungumuzo yetu na kila hali. Hata ikiwa namna mbalimbali za kuanzisha mazungumuzo zimependekezwa, wahubiri wanaweza kubadilisha ao kutayarisha utangulizi wao wenyewe. Kwa hiyo, tutapata matokeo mazuri ikiwa tunatayarisha muzuri maneno yetu ya utangulizi kuliko kusema tu maneno ambayo yanatufikia katika akili wakati musikilizaji anafungua mulango.—Met. 15:28.
Namna ya Kufanya:
• Chagua habari utakayozungumuzia. Inapashwa kutoka katika kichapo tunachowatolea watu na inapashwa kuwapendeza watu katika eneo letu.
• Tayarisha muzuri maneno mafupi ya kwanza-kwanza utakayosema kisha kumusalimia musikilizaji. Unaweza kuanzisha mazungumuzo kwa kusema hivi: “Ninawatembelea kwa sababu ya . . . ,” “Watu wengi wanahangaikia . . . ,” “Unawaza nini kuhusu . . . ,” ao namna ingine. Mara nyingi, maneno mafupi na yenye kueleweka yana matokeo mazuri. Wahubiri fulani wanaamua kuweka katika akili maneno yao ya utangulizi.
• Uliza ulizo litakalomuchochea musikilizaji atoe maoni yake ili kuendelesha mazungumuzo. (Mt. 17:25) Usisahau kwamba pengine musikilizaji alikuwa akifiria mambo mengine mbele ufike kumutembelea. Kwa hiyo, usimuulize ulizo ngumu sana ao ulizo litakalomufanya ajisikie kwamba hajue kitu.
Tumikisha Shauri Hili Katika Mwezi:
• Munapofanya ibada ya familia, mutumie wakati fulani ili kutayarisha na kufanya mazoezi ya maneno yenu ya utangulizi.
• Unapokuwa katika mahubiri, waelezee wahubiri wengine maneno ya utangulizi ambayo umepanga kutumia. (Met. 27:17) Badilisha maneno yako ya utangulizi ikiwa haupate matokeo mazuri.