Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwb16 Mwezi wa 3 uku. 8
  • Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri—Kuandika Namna Yako ya Kuwatolea Watu Magazeti

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri—Kuandika Namna Yako ya Kuwatolea Watu Magazeti
  • Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2016
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Kutayarisha Namna ya Kutolea Mtu Gazeti
    Huduma Yetu ya Ufalme—2006
  • Jinsi ya Kutumia Utoaji Mbalimbali Wenye Kupendekezwa
    Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Tolea Watu Magazeti Yanayotoa Ushahidi Juu ya Ile Kweli
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Namna ya Kuanzisha Mazungumuzo
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2018
Ona Habari Zaidi
Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2016
mwb16 Mwezi wa 3 uku. 8

TUJITOE KABISA KATIKA KAZI YA KUHUBIRI

Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri—Kuandika Namna Yako ya Kuwatolea Watu Magazeti

Maandishi
Mashahidi wa Yehova wanazungumuzia habari fulani ya gazeti pamoja na mwanaume

SABABU GANI NI LAZIMA KUFANYA HIVYO: Hata kama sehemu za namna ya kuanzisha mazungumuzo zenye kuwa katika buku la mukutano zinatupatia mawazo yenye kutusaidia sana, usisahau kwamba sehemu hizo ni mifano tu. Unapaswa kutumia maneno yako mwenyewe. Unaweza kutumia namna ingine ya kuanzisha mazungumuzo ao unaweza kuona kwamba habari ingine inaweza kuwavutia zaidi watu katika eneo. Kama ni hivyo, kisha kusoma gazeti, kuchunguza namna za kuanzisha mazungumuzo, na kuona video za kuonyesha namna ya kuanzisha mazungumuzo, unaweza kutumia mapendekezo yenye kufuata ili kuandika namna yako ya kuanzisha mazungumuzo.

NAMNA YA KUFANYA:

Ujiulize, ‘Je, nitumie moja kati ya mifano ya namna ya kuanzisha mazungumuzo?’

NDIYO

  • Utayarishe maneno yako ya utangulizi. Kisha kumusalimia musikilizaji, umuambie kwa kifupi sababu gani unamutembelea. (Unaweza kusema: “Nakutembelea kwa sababu . . . ”)

  • Uchague maneno yenye utasema kisha kumuuliza mutu ulizo, kumusomea andiko na kumutolea kichapo. (Mbele ya kusoma andiko unaweza kusema: “Jibu la ulizo hilo linapatikana katika andiko hili.”)

HAPANA

  • Uchague habari moja ya gazeti yenye kukupendeza na yenye itavutia watu wa eneo

  • Utayarishe ulizo lenye litamuchochea mutu atoe mawazo yake, lakini lenye halitamufanya ajisikie mubaya. (Kwa mufano unaweza kutumia maulizo yenye kuwa kwenye ukurasa wa 2 wa magazeti.)

  • Uchague andiko la kusoma. (Kama unamutolea mutu Amuka! unaweza kusoma andiko ao hapana, kwa sababu gazeti Amuka! inahusu watu wenye hawajue mambo mengi juu ya Biblia na pengine hawatumainie dini.)

  • Uchague maneno fulani yenye kumuonyesha musikilizaji faida yenye atapata kwa kusoma habari yenye unamutolea

  • Utayarishe ulizo lenye utamuachia ili kulijibia wakati utamurudilia

  • Andika mambo fulani yenye itakusaidia kukumbuka maneno yenye ulipanga kusema

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine