Mwezi wa 8 Utakuwa Mwezi wa Pekee Sana Kwa Ajili ya Mahubiri!
Tutawatolea Watu Trakte Mupya Duniani Pote
1. Ufalme unapokaribia kutimiza miaka 100, ni kampanye gani ya pekee itakayofanywa duniani pote?
1 Ufalme wa Mungu unakaribia kutimiza miaka 100 tangu ulipoanza kutawala; kwa hiyo, tuna nafasi nzuri ya kumutukuza Yehova kupitia kampanye ya pekee. Katika Mwezi wa 8 tutawatolea watu duniani pote trakte mupya yenye kichwa: “Ni wapi unaweza kupata majibu ya maulizo ya maana sana kuhusu maisha?” Trakte hii inawatia moyo wasomaji watumie Biblia ili kupata majibu na inaeleza namna gani adresi yetu ya Internete jw.org inaweza kuwasaidia.
2. Namna gani tunaweza kushiriki katika ‘kupaaza sauti kubwa ya kumusifu Yehova’ katika Mwezi wa 8?
2 Tupaaze Sauti Kubwa ya Sifa: Ili kuwasaidia ndugu na dada wahubiri zaidi, mupango wa pekee umefanywa ili kila muhubiri anayetaka awe painia musaidizi katika Mwezi wa 8. Katika mwezi huo, wahubiri waliobatizwa watapewa nafasi ya kuwa mapainia wasaidizi wa saa 30. Kwa kuwa Mwezi wa 8 utakuwa na Siku za Tano 5, Siku za Posho 5, na Siku za Yenga 5, wahubiri wengi ambao ni wafanyakazi ao wale wanaenda kwenye masomo katika juma, wanaweza kuwa mapainia wasaidizi. Ikiwa una mwanafunzi fulani wa Biblia anayetimiza mambo yanayoombwa ili kuwa muhubiri ao mutoto anayependa kuwa muhubiri, mujulishe muratibu wa baraza la wazee wa kutaniko lenu bila kukawia. Tutafurahi na kutiwa moyo sana ikiwa watu hao watajiunga na sisi katika kuhubiri katika mwezi huo wa pekee sana. Hata kama mapainia wengi wanachukua mapumuziko katika Mwezi wa 8 kisha kueneza saa ambazo wanaombwa kwa mwaka, wanaweza kubadilisha programu zao ili washiriki kwa bidii katika kampanye hiyo ya pekee. Sasa huu ndiyo wakati familia zinaweza kupanga namna watashiriki ‘kupaaza sauti kubwa ya kumusifu Yehova’ ambayo itafanywa katika Mwezi wa 8.—Ezra 3:11; Met. 15:22.
3. Tuko na tumaini gani kuhusu kampanye hii ya pekee?
3 Hata ikiwa tumeshiriki katika kampanye mbalimbali kama hii wakati uliopita, tunatumaini kwamba kampanye hii itakuwa ya pekee sana. Je, tutatumia nafasi hiyo ili kuongeza hesabu ya saa, wahubiri na mapainia wasaidizi katika Mwezi wa 8? Tunapofikia mwisho wa mwaka wa utumishi wa 2014, tunatumaini kwamba Yehova atabariki bidii ya watumishi wake duniani pote ili watoe ushahidi mukubwa zaidi katika Mwezi wa 8.—Mt. 24:14.