Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 9/14 uku. 2
  • Tuige Mufano wa Manabii—Nahumu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tuige Mufano wa Manabii—Nahumu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Habari Zenye Kuwa Katika Nahumu
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • Ulijua?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
Huduma Yetu ya Ufalme—2014
km 9/14 uku. 2

Tuige Mufano wa Manabii—Nahumu

1. Kitabu cha Nahumu kinatufundisha nini?

1 Kuharibiwa kwa muji wa zamani wa Ninawi kunaonyesha kabisa kwamba, kama vile nabii Nahumu alitabiri, Yehova analipiza kisasi juu ya adui zake na kwamba hata adui zake wawe na nguvu nyingi, hawawezi hata kidogo kusimama mbele Yake. (Nah. 1:2, 6) Kuchunguza kwa uangalifu unabii wa Nahumu kunatufundisha mambo mengi leo kuhusu kazi yetu ya mahubiri.

2. Tunaweza kufanya nini ili ujumbe wetu uendelee kuwa wenye kutia moyo?

2 Tutie Watu Moyo na Tuwatolee Tumaini: Ukichunguza haraka haraka kitabu cha Nahumu, kinaweza kuonekana tu kuwa kitabu chenye ujumbe wa hukumu juu ya Ninawi, muji mukubwa na wenye kuvutia wa Ashuru ya zamani. (Nah. 1:1; 3:7) Hata hivyo, tangazo hilo lilikuwa habari njema kwa watu wa Yehova. Nahumu, ambaye jina lake linamaanisha “Mutia-moyo,” aliwahakikishia Wayahudi kwamba karibuni maadui wao wataangamizwa! Tena, Nahumu alihakikisha kwamba Yehova ni “ngome katika siku ya taabu.” (Nah. 1:7) Sisi pia, wakati tunahubiri tunatangazia watu habari njema na kuwatia moyo watafute kimbilio kwa Yehova.—Nah. 1:15.

3. Namna gani tunaweza kumuiga Nahumu katika kutumia mifano mbalimbali?

3 Tumia Mifano Mbalimbali: Kwa musaada wa roho ya Yehova, Nahumu alilinganisha uharibifu wa Ninawi na ule wa muji wa Misri unaoitwa Thebes (ao No-amon), ambao Waashuru wenyewe walikuwa wameharibu. (Nah. 3:8-10) Wakati tunawahubiria watu kuhusu uharibifu wa ulimwengu huu muovu, tunaweza kukazia unabii mbalimbali wa Biblia ambao unashuhudia kwamba Yehova anatimiza unabii wake bila kukosea hata katika jambo moja. Kwa mufano, wakati Wababiloni na Wamedi walifika ili kuangamiza jiji la Ninawi katika mwaka wa 632 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, mvua kubwa ulifanya muto wa Tigri ujae sana, na maji hayo yakabomoa sehemu fulani ya kuta zenye nguvu za muji huo. Kama vile Yehova alitabiri, muji wa Ninawi ulikamatwa haraka.—Nah. 1:8; 2:6.

4. Namna gani tunaweza kutumia maneno yaliyo wazi na yenye kueleweka katika mahubiri?

4 Tutumie Maneno Yaliyo Wazi na Yenye Kueleweka: Nahumu aliandika kitabu chake kwa njia ya kueleza mambo na yenye kufanya mutu aone katika akili mambo yanayoelezwa. Habari aliyoeleza ilikuwa wazi. (Nah. 1:14; 3:1) Sisi pia tunapaswa kutumia maneno yenye kueleweka kwa urahisi. (1 Kor. 14:9) Wakati unatembelea mutu fulani mara ya kwanza, muambie wazi wazi sababu gani unamutembelea. Wakati unajifunza Biblia na mutu fulani, umusaidie akomalishe imani yake katika Yehova na Neno lake na umusaidie atambue faida ya kutumikisha mambo ambayo anajifunza katika maisha yake.—Rom. 10:14.

5. Unabii wa Nahumu unatuhakikishia nini?

5 Kitabu cha Nahumu kinaonyesha wazi kwamba nabii huyo alikuwa na tumaini lenye nguvu katika utimizo wa maneno ya Yehova. Kwa kuwa mwisho wa ulimwengu wa Shetani unakaribia, tunatiwa moyo na maneno haya ya Mungu: “Taabu haitazuka [haitatokea] mara ya pili.”—Nah. 1:9.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine