Tutumie jw.org Katika Mahubiri—“Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa”
Unapofungua sehemu “Mafundisho ya Biblia” kwenye jw.org, utaona habari yenye kichwa “Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa.” Tukijikaza kujua maulizo hayo yanayoulizwa mara kwa mara, wakati musikilizaji anatuuliza ulizo fulani kati ya maulizo hayo, tutakuwa tayari kumuonyesha namna ya kupata jibu la Biblia la ulizo hilo kwenye jw.org. Tunaweza pia kutumia maulizo hayo ili kuanzisha mazungumuzo katika mahubiri. Tunaweza kuchagua ulizo moja linalowavutia watu katika eneo letu, kuomba musikilizaji atoe maoni yake juu ya ulizo hilo, na kisha tunaweza kumuambia yale ambayo Biblia inasema kwa kutumia jibu lililo kwenye jw.org. Kisha tunaweza kumufasiria ao kumuonyesha namna tulipata jibu hilo. Ao tunaweza kumuacha ajisomee jibu moja kwa moja kwenye jw.org. Bibi ya mwangalizi mumoja amepata matokeo mazuri kwa kusema hivi: “Watu wengi wanajiuliza ikiwa ‘Mungu ndiye analetea watu mateso.’ Ungependa kusikia jibu kwa segonde 51?” Kisha anamuomba musikilizaji asikilize jibu alilochukua kwenye jw.org katika smartphone yake. Anamaliza kwa kumuonyesha sura ya 11 ya kitabu Biblia Inafundisha.