Tutiane Moyo kwa Bidii Katika Matendo Mazuri
Andiko la Waebrania 10:24 linatuomba ‘tuchocheane [tutiane moyo] katika upendo na matendo mazuri.’ Tunaweza kuwatia moyo ndugu na dada zetu kupitia mufano wetu na maneno yetu. Elezea ndugu na dada katika kutaniko mambo mazuri yenye ulijionea katika maisha yako ya Kikristo. Waonyeshe furaha yenye umepata katika kumutumikia Yehova. Lakini, epuka kujilinganisha nao ao kuwalinganisha na watu wengine kwa njia isiyofaa. (Gal. 6:4) Tafuta nafasi ya kutumia uwezo wako ili kuwatia wengine moyo katika “upendo na matendo mazuri,” hapana katika kuwahukumu na matendo mazuri. (Soma kitabu Shule ya Huduma, uku. 158, fu. 4.) Kwanza, tuchochee wengine katika upendo; kisha, matendo, kama vile kuwafanyia wengine mema ao kuwahubiri, yatafuata.—2 Kor. 1:24.