Tumia Nguvu za Neno la Mungu Katika Mahubiri
Wakati tunapata nafasi ya kuzungumuza na mutu juu ya habari njema, ni muzuri kutumia nguvu za neno la Mungu kwa kumusomea moja kwa moja maandiko katika Biblia. Jambo hilo lilikaziwa sana kwenye mukusanyiko wetu wa pekee wa 2014. Mwangalizi wa muzunguko alitoa hotuba yenye kichwa “Tumia Nguvu za Neno la Mungu Katika Mahubiri.” Unakumbuka mambo makubwa ya hotuba hiyo?
Sababu gani neno la Yehova liko na nguvu kuliko maneno yetu?—2 Tim. 3:16, 17.
Namna gani Biblia inagusa mioyo ya watu, inabadilisha mawazo yao, inafanya nia na tabia zao kuwa nzuri zaidi?—Ona Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 6, 2012, uku. 27, fu. 7.
Wakati tunamusomea mutu andiko fulani katika mahubiri, namna gani tunaweza kuelekeza uangalifu kwenye Neno la Mungu ili mutu huyo aliheshimie?—Ona kitabu Shule ya Huduma, uku. 148, fu. 3-4 na Huduma Yetu ya Ufalme ya Mwezi wa 3, 2013, uku. 6, fu. 8.
Sababu gani ni jambo la lazima kutoa maelezo na kufikiri sana na musikilizaji juu ya maandiko yenye mumesoma, na namna gani tunaweza kufikia kufanya hivyo—Mdo. 17:2, 3; Ona kitabu Shule ya Huduma, uku. 154, fu. 4 mupaka uku. 156, fu. 5.