Jinsi ya Kuanzisha Mafunzo Katika Kitabu Biblia Inafundisha
Wengi kati yetu wangependezwa kuongoza funzo la Biblia, lakini tatizo ni namna gani wangeweza kulianzisha. Kitabu kipya Biblia Inafundisha Nini Hasa? kinaweza kutusaidia. Utangulizi kwenye ukurasa wa 3-7 una kusudi la kuvutia mwenye nyumba ili ashiriki katika mazungumzo ya Biblia tukitumia kitabu. Hata wale wasio na uzoefu mwingi katika huduma wataona kwamba ni rahisi kutumia kitabu hicho ili kuanzisha mafunzo.
◼ Unaweza kujaribu utangulizi huu ukitumia ukurasa wa 3:
Baada ya kutaja habari au tatizo lililo katika akili ya watu wa eneo lenu, elekeza uangalifu wa mwenye nyumba kwenye maulizo yanayoandikwa kwa herufi nzito nyeusi kwenye ukurasa wa 3, na umwombe atoe maelezo. Kisha fungua kwenye ukurasa wa 4-5.
◼ Au unaweza kupendelea kuanza kwa kukazia ukurasa wa 4-5:
Unaweza kusema, “Je, halingekuwa jambo nzuri ajabu ikiwa mabadiliko yanayoonyeshwa hapa yangefanyika kweli?” Au unaweza kuuliza, “Ni ahadi gani kati ya hizo ungependa kuona itimizwe?” Sikiliza jibu la mwenye nyumba kwa uangalifu.
Ikiwa mwenye nyumba anaonyesha kupendezwa kwa pekee na andiko moja, mwonyeshe yale ambayo Biblia inafundisha kuhusu habari hiyo mkichunguza mafungu yanayozungumzia andiko hilo katika kitabu. (Ona kisanduku kwenye ukurasa huu wa nyongeza.) Chunguza habari hiyo kama vile tu ungefanya kwenye funzo la Biblia. Jambo hilo linaweza kufanywa katika dakika tano au kumi kwenye ziara ya kwanza mkiwa mlangoni.
◼ Utangulizi mwingine ni kumfanya mtu atoe mawazo yake ukitumia ukurasa wa 6:
Elekeza uangalifu wa mwenye nyumba kwenye maulizo yaliyo chini ya ukurasa, na uliza, “Je, umekwisha kujiuliza kuhusu lolote kati ya maulizo hayo?” Ikiwa anaonyesha kupendezwa na moja la maulizo, fungua kitabu kwenye mafungu yanayojibu ulizo hilo. (Ona kisanduku kwenye ukurasa huu wa nyongeza.) Mnapochunguza habari pamoja, tayari wewe ni mwenye kuongoza funzo la Biblia.
◼ Ukurasa wa 7 unaweza kutumiwa ili kufanya onyesho la funzo la Biblia:
Soma sentensi tatu za mwanzo kwenye ukurasa huo, na kisha fungua kwenye sura ya 3 na fanya onyesho la funzo ukitumia fungu la 1-3. Fanya mpango ili kurudi kuzungumzia majibu ya maulizo katika fungu la 3.
◼ Jinsi ya kufanya mpango wa ziara ya kurudia:
Unapomalizia funzo la kwanza, fanya mpango ili kuendeleza mazungumzo. Unaweza tu kusema: “Kwa dakika chache tu, tumejifunza yale Biblia inayofundisha kuhusu habari ya maana. Nitakaporudi tena, tunaweza kuzungumzia [acha ulizo litakalozungumziwa]. Je, ninaweza kurudi juma lijalo wakati kama huu?”
Tunapokaribia sana wakati uliowekwa na Yehova, yeye anaendelea kututolea vifaa tunavyohitaji kwa ajili ya kazi tunayo. (Mt. 28:19, 20; 2 Tim. 3:17) Acheni sisi tutumie vizuri chombo hicho kipya ili kuanzisha mafunzo ya Biblia.
[Kisanduku Kwenye Ukurasa wa 3]
Mazungumzo Yanayotegemea Maandiko Kwenye Ukurasa wa 4-5
◻ Ufunuo 21:4 (uku. 27-28, fu. 1-3)
◻ Isaya 33:24; 35:5, 6 (uku. 36, fu. 22)
◻ Yohana 5:28, 29 (uku. 72-73, fu. 17-19)
◻ Zaburi 72:16 (uku. 34, fu. 19)
Majibu ya Maulizo, Ukurasa wa 6
◻ Kwa nini tunateseka? (uku. 108-109, fu. 6-8)
◻ Tunawezaje kupambana na mahangaiko ya maisha? (uku. 184-185, fu. 1-3)
◻ Tunawezaje kufanya maisha ya familia yetu yawe yenye furaha zaidi? (uku. 143, fu. 20)
◻ Inakuwaje tunapokufa? (uku. 58-59, fu. 5-6)
◻ Je, tutapata kuwaona tena wapendwa wetu waliokufa? (uku. 72-73, fu. 17-19)
◻ Tunawezaje kuwa hakika kwamba Mungu atatimiza ahadi zake kuhusu wakati ujao? (uku. 24, fu. 17)