Je, Utaanzisha Funzo la Biblia Katika Mwezi wa 10?
1. Tutatolea watu nini mwezi wa 10?
1 Mwezi wa 10 tutatolea watu Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Ili kufuatia kupendezwa, tunatiwa moyo kutolea watu trakti Je, Ungependa Kujua Kweli? na kujikaza kuanzisha funzo la Biblia. Namna gani tunaweza kufanya hivyo tunaporudilia wale waliopendezwa?
2. Namna gani tunaweza kutumia trakti Kujua Kweli ili kuanzisha funzo la Biblia tunaporudilia mutu aliyekubali magazeti?
2 Jinsi ya Kutumia Trakti Hiyo: Tunaweza kusema: “Magazeti ambayo nilikuachia yanatia moyo watu wa hali zote na dini zote wachunguze Biblia. [Mtolee msikilizaji trakti Kujua Kweli, na uonyeshe maulizo yaliyo kwenye ukurasa wa mwanzo.] Haya ni maulizo ya maana sana ambayo Biblia inatoa majibu yenye kutosheleza. Je, umekwisha kujiuliza ulizo lolote kati ya maulizo haya?” Msikilizaji akisha kujibu, muchunguze pamoja jibu la ulizo lake kutoka trakti, na usome andiko moja kati ya maandiko yanayotajwa. Kisha umuonyeshe kwamba huo ni mfano mmoja tu wa mambo ambayo Biblia inafundisha, na umuachie kitabu Biblia Inafundisha. Kwa hiyo, tunaweza kujifunza mafungu ya mwanzo ya sura ambayo atachagua kutoka ukurasa wa 2 (Yaliyomo). Ao tunaweza kutafuta kitabu kingine kilicho na habari zaidi kuhusiana na habari tuliyozungumzia katika trakti. Tunaweza kutumia Trakti Kujua Kweli ili kuanzisha funzo katika kitabu Biblia Inafundisha kama inavyoonyeshwa hapa chini:
● Je, kweli Mungu anatuhangaikia? (uku. 9-11, fu. 6-10)
● Je, vita na mateso vitakwisha wakati wowote? (uku. 12, fu. 12-13)
● Ni jambo gani linalotupata tunapokufa? (uku. 59-60, fu. 7-8)
● Je, kuna tumaini lolote kwa wafu? (uku. 71, fu. 13-15)
● Namna gani ninaweza kusali ili Mungu anisikie? (uku. 166-167, fu. 5-8)
● Ninaweza kufanya nini ili nipate furaha maishani? (uku. 9, fu. 4-5)
3. Namna gani tunaweza kubadili utoaji wetu kulingana na hali?
3 Bila shaka, ikiwa hali hazituruhusu kuanzisha na kuonyesha jinsi funzo linafanyika katika kitabu Biblia Inafundisha tunaporudilia waliopendezwa kwa mara ya kwanza, tunaweza kufanya mipango ya kurudi na kuendelesha mazungumzo. Na kulingana na jinsi mutu anavyopendezwa, tunapomrudilia tunaweza kuendelea kuzungumzia kwanza maulizo mawili ao zaidi kutoka katika trakti mbele ya kutumia kitabu. Acheni tutumie vizuri trakti hii ya maana sana katika mwezi wa 10 ili kuanzisha funzo la Biblia na kuwasaidia watu wenye mioyo yenye haki ‘kuijua kweli.’—Yoh. 8:31, 32.