Namna Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
Munara wa Mulinzi 01/05
“Kama ungekuwa na uwezo wa kumaliza magumu fulani katika dunia, ungechagua kumaliza magumu gani? [Acha mutu ajibu.] Kulingana na Biblia, karibuni Mungu atamaliza tatizo hiyo na matatizo mengine pia. [Soma andiko moja lenye kupatana na hali yake kati ya maandiko haya: Danieli 2:44; Methali 2:21, 22; Mathayo 7:21-23; ao 2 Petro 3:7.] Gazeti hili linazungumuzia wakati na namna gani Mungu ataleta mabadiliko kama hayo juu ya dunia.”
Amuka! Mwezi wa 5
“Unawaza kama itawezekana siku moja tuishi katika dunia yenye haitakuwa tena na watu masikini na kila mutu atakuwa na nyumba nzuri? [Acha mutu ajibu.] Tafazali ona ahadi yenye Mungu anatutolea. [Soma Isaya 65:21, 22.] Gazeti hili linaonyesha namna Mungu atatimiza ahadi yake kuhusu wanadamu na namna gani tunaweza kufaidika na ahadi hiyo.”