Elifazi:
Pengine alitoka katika muji wa Temani katika inchi ya Edomu. Kulingana na andiko la Yeremia 49:7, Temani lilikuwa eneo lenye kujulikana sana la hekima ya Edomu
Inawezekana Elifazi alikuwa mukubwa na mwenye kujulikana sana kuliko “wafariji” wengine, alikuwa wa kwanza kusema. Alisema mara tatu na maneno yake yalikuwa marefu kuliko ya wengine wawili
Mashitaka yake ya uwongo kuhusu Ayubu:
Alizarau uaminifu wa Ayubu na alisema kwamba Mungu hatumainie watumishi wake (Ayubu sura ya 4 na 5)
Alisema Ayubu ni mwenye kiburi na muovu na hamuogope Mungu hata kidogo (Ayubu sura 15)
Alisema kwamba Ayubu ni mwenye pupa na hafuatilie haki na aliongeza kwamba mwanadamu hana faida yoyote kwa Mungu (Ayubu sura ya 22)
Bildadi:
Mashitaka yake ya uwongo kuhusu Ayubu:
Alisema kwamba watoto wa Ayubu walikuwa watenda-zambi na kwamba walistahili kupata musiba wenye uliwafikia na alisema kwamba Ayubu mwenyewe hakumuogopa Mungu (Ayubu sura ya 8)
Alisema kwamba Ayubu alikuwa mutenda-zambi (Ayubu sura ya 18)
Alisema kwamba uaminifu wa mwanadamu hauna faida yoyote (Ayubu sura ya 25)
Sofari:
Alikuwa Munaamathi, pengine alitoka kaskazini-mangaribi ya Arabia
Alikuwa wa tatu kusema na maneno yake yalikuwa makali zaidi kuliko ya wengine wote. Alisema mara mbili tu
Mashitaka yake ya uwongo kuhusu Ayubu: