Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwb16 Mwezi wa 4 uku. 3
  • Utie Wengine Moyo Kupitia Maneno Yenye Upendo ili Wapate Nguvu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Utie Wengine Moyo Kupitia Maneno Yenye Upendo ili Wapate Nguvu
  • Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2016
  • Habari za Kufanana na Zile
  • “Sitaacha Uaminifu-Mushikamanifu Wangu!”
    Tuige Imani Yao
  • Kusali kwa Ajili ya Wengine Kunamupendeza Yehova
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2016
  • Habari Zenye Kuwa Katika Yobu
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • “Umutumainie Yehova”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2016
mwb16 Mwezi wa 4 uku. 3

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | AYUBU 16-20

Utie Wengine Moyo Kupitia Maneno Yenye Upendo ili Wapate Nguvu

Wakati unafariji wengine, tumia maneno yenye kuwatia nguvu

16:4, 5

  • Kwa sababu Ayubu alikuwa mwenye kuvunjika moyo na mwenye kuhangaika, alihitaji musaada na maneno ya wengine yenye kutia moyo

  • Marafiki watatu wa Ayubu hawakusema maneno ya kumufariji. Lakini, walisema maneno ya kumuhukumu yenye yaliongeza mahangaiko yake

Maneno ya Bildadi ya kuvunja moyo yalifanya Ayubu alie sana

19:2, 25

  • Ayubu alililia Mungu amutulize kwa njia fulani, hata kupitia kifo

  • Ayubu alikazia akili yake juu ya tumaini la ufufuo na aliendelea kuvumilia kwa uaminifu

Elifazi anasema na Ayubu, na Sofari na Bildadi wanawaangalia

WACHONGEZI WA AYUBU

Elifazi

Elifazi:

  • Pengine alitoka katika muji wa Temani katika inchi ya Edomu. Kulingana na andiko la Yeremia 49:7, Temani lilikuwa eneo lenye kujulikana sana la hekima ya Edomu

  • Inawezekana Elifazi alikuwa mukubwa na mwenye kujulikana sana kuliko “wafariji” wengine, alikuwa wa kwanza kusema. Alisema mara tatu na maneno yake yalikuwa marefu kuliko ya wengine wawili

Mashitaka yake ya uwongo kuhusu Ayubu:

  • Alizarau uaminifu wa Ayubu na alisema kwamba Mungu hatumainie watumishi wake (Ayubu sura ya 4 na 5)

  • Alisema Ayubu ni mwenye kiburi na muovu na hamuogope Mungu hata kidogo (Ayubu sura 15)

  • Alisema kwamba Ayubu ni mwenye pupa na hafuatilie haki na aliongeza kwamba mwanadamu hana faida yoyote kwa Mungu (Ayubu sura ya 22)

Bildadi

Bildadi:

  • Alizaliwa katika kizazi cha Shua. Pengine aliishi karibu na Muto Efrati

  • Alikuwa wa pili kusema. Maneno yake matatu yalikuwa mafupi lakini yenye kuumiza zaidi kuliko maneno ya Elifazi

Mashitaka yake ya uwongo kuhusu Ayubu:

  • Alisema kwamba watoto wa Ayubu walikuwa watenda-zambi na kwamba walistahili kupata musiba wenye uliwafikia na alisema kwamba Ayubu mwenyewe hakumuogopa Mungu (Ayubu sura ya 8)

  • Alisema kwamba Ayubu alikuwa mutenda-zambi (Ayubu sura ya 18)

  • Alisema kwamba uaminifu wa mwanadamu hauna faida yoyote (Ayubu sura ya 25)

Sofari

Sofari:

  • Alikuwa Munaamathi, pengine alitoka kaskazini-mangaribi ya Arabia

  • Alikuwa wa tatu kusema na maneno yake yalikuwa makali zaidi kuliko ya wengine wote. Alisema mara mbili tu

Mashitaka yake ya uwongo kuhusu Ayubu:

  • Alisema kwamba maneno ya Ayubu yalikuwa ya upumbavu na alimuambia aache matendo yake mabaya (Ayubu sura ya 11)

  • Alisema kwamba Ayubu alikuwa muovu na alipenda kufanya zambi (Ayubu sura ya 20)

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine