Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp20 na. 3 uku. 4-5
  • Muumbaji Wetu Mwenye Upendo Anatuhangaikia

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Muumbaji Wetu Mwenye Upendo Anatuhangaikia
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2020
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • 1. MUUMBAJI WETU ANAFANYA JUA LITUANGAZIE
  • 2. MUUMBAJI WETU ANATUPATIA MVUA
  • 3. MUUMBAJI WETU ANATUPATIA CHAKULA NA NGUO
  • Tafuta Ufalme, Usitafute Vitu vya Kimwili
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
  • Muumba Wetu Mtukufu Anatujali!
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Juu ya Nini Ni Jambo ya Maana Kuamini Kama Kuko Muumbaji?
    Amuka!—2021
  • Angalia Ndege kwa Uangalifu
    Amuka!—2014
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2020
wp20 na. 3 uku. 4-5
Jua linatokea ngambo ya mulima.

Muumbaji Wetu Mwenye Upendo Anatuhangaikia

1. MUUMBAJI WETU ANAFANYA JUA LITUANGAZIE

Unawaza maisha ingekuwa namna gani ku dunia bila mwangaza wa jua? Jua linasaidia miti itoe majani, maua, matunda, na mbegu. Linasaidia pia miti ikokote maji mu udongo kupitia mizizi na kuipandisha mupaka ku majani na kisha mu anga na imekuwa muvuke.

Namna shamba la chai linaonekana ku mulima, wakati mutu analiangalia kwa juu.

2. MUUMBAJI WETU ANATUPATIA MVUA

Mvua ni zawadi ya muzuri yenye Mungu anatupatia, na inasaidia dunia itutolee chakula. Mungu anatupatia mvua kutoka mbinguni na vipindi vya kuzaa matunda, na anatupatia chakula kwa wingi na kujaza mioyo yetu furaha.

Ndege yenye kuwa ku tawi iko inatafuta kukamata tunda lenye linataka kuanguka.

3. MUUMBAJI WETU ANATUPATIA CHAKULA NA NGUO

Mambo yenye inahangaisha baba wengi ni kupata chakula na nguo zenye watu wa familia wako nazo lazima. Ona mambo yenye Maandiko inasema: “Muangalie kwa uangalifu ndege wa mbinguni; hawapande mbegu ao kuvuna ao kukusanya katika madepo, lakini Baba yenu wa mbinguni anawalisha. Je, ninyi hamuko wa maana kuliko wao?”​—Matayo 6:25, 26.

“Muangalie muzuri maua ya mayungiyungi ya shamba, namna yanakomaa . . . ; lakini mimi ninawaambia kwamba hata [Mufalme] Sulemani katika utukufu wake wote hakupambwa kama moja ya maua hayo. Basi, kama ni vile Mungu anavalisha mimea yenye kuwa katika shamba . . . , je, hatawavalisha muzuri zaidi?”​—Matayo 6:28-30.

Juu Mungu iko na uwezo wa kutupatia chakula na nguo, bila shaka iko pia na uwezo wa kutupatia mambo ingine yenye tuko nayo lazima. Kama tunafanya mapenzi ya Mungu, anaweza kubariki bidii yenye tunafanya ili kulima chakula ao anaweza kutusaidia tupate kazi ya kutusaidia tuuze mambo yenye tuko nayo lazima.​—Matayo 6:32, 33.

Tuko na sababu za muzuri za kumupenda Mungu wakati tunafikiria jua, mvua, ndege, na maua. Habari yenye kufuata itazungumuzia namna Mungu amezungumuza na wanadamu.

Muumbaji wetu “anaangazia jua lake . . . tena ananyesha mvua.”​—MATAYO 5:45

Muumbaji wetu anatupenda sana na kutuhangaikia. Anahangaikia familia yake kama vile baba mwenye upendo. Maandiko Matakatifu inasema kama Mungu ni Mutoaji mukarimu mwenye ‘anajua kile chenye uko nacho lazima hata mbele umuombe.’​—Matayo 6:8.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine