Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwb18 Mwezi wa 3 uku. 8
  • Namna ya Kukomalisha Upendo Wetu kwa Mungu na kwa Jirani

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Namna ya Kukomalisha Upendo Wetu kwa Mungu na kwa Jirani
  • Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2018
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mambo ya Kufanya juu Ufaidike na Usomaji Wako wa Biblia
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
  • Unaweza Kufanya Nini Juu Upate Faida Wakati Uko Nasoma Biblia
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Juu ya Nini Kusoma Ni Jambo ya Maana kwa Watoto​—Sehemu ya 1: Kusoma ao Kuangalia?
    Musaada kwa Familia
Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2018
mwb18 Mwezi wa 3 uku. 8

MAISHA YA MUKRISTO

Namna ya Kukomalisha Upendo Wetu kwa Mungu na kwa Jirani

Hata kama Wakristo hawafuate tena Sheria ya Musa, zile amri mbili kubwa zaidi za Sheria hiyo, ni kusema, kumupenda Mungu na kumupenda jirani, ni kifupi cha mambo yote yenye Yehova anatuomba. (Mt 22:37-39) Hatuzaliwe na upendo huo. Tunapaswa kuukomalisha. Namna gani? Moja kati ya njia za lazima zaidi ni kusoma Biblia kila siku. Wakati tunawaza sana juu ya sifa mbalimbali za Mungu zenye tunasoma katika Biblia, tunajionea “uzuri wa Yehova.” (Zab 27:4) Hilo linafanya upendo wetu kwake ukomae na tuanze kuona mambo kama yeye. Kwa kufanya hivyo, tunachochewa kutii amri za Mungu, kwa mufano amri ya kuonyesha wengine upendo wa kujizabihu. (Yoh 13:34, 35; 1Yoh 5:3) Mapendekezo haya tatu inaweza kutusaidia tufurahie zaidi usomaji wetu wa Biblia:

  • Tumia uwezo wako wa kufikiri, na hisia zako. Wazia kama uko hapo. Ona, sikia sauti, na harufu. Ujiulize: Watu wenye kuzungumuziwa walijisikia namna gani?

    Ndugu anafikiri juu ya mambo yenye anasoma katika Biblia
  • Badilisha namna yako ya kusoma. Mapendekezo fulani: Soma kwa sauti, ao sikiliza rekodi kwa kufuata katika Biblia yako. Kuliko kusoma sura namna zinafuatana, soma juu ya mutu ao habari fulani. Kwa mufano, ili kupata habari zaidi juu ya Yesu, tumia Nyongeza A7 ao B12 katika Biblia Takatifu​—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya, ao sehemu ya 4 ao ya 16 ya broshua Musaada wa Kujifunza Neno la Mungu. Soma sura yote mwenye andiko la siku lilichukuliwa. Soma vitabu vya Biblia kufuatana na wakati viliandikwa.

    Dada anasoma Biblia kwenye jw.org
  • Soma na kusudi la kuelewa. Ni muzuri zaidi kusoma hata sura moja kila siku na kuielewa na kufikiri sana, kuliko kusoma sura nyingi ili tu kumaliza habari zenye tunasoma. Chunguza ni katika hali gani habari iliandikwa. Chunguza hata mambo madogo-madogo. Tumia karte na michoro na pia maelezo ya pembeni ao ya katikati. Ujikaze kutafuta hata jambo moja lenye hauelewe. Kama inawezekana, tumia wakati uleule ili kuwaza sana juu ya mambo yenye unasoma.

    Nyongeza mbili za Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine