UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MARKO 13-14
Epuka Kuangukia Katika Mutego wa Kuogopa Mwanadamu
Sababu gani mitume waliangukia katika mutego wa kuogopa mwanadamu?
Walijitumainia kupita kiasi. Petro alimuhakikishia Yesu kama angebakia mushikamanifu kwake hata kama mitume wengine wote wangemuacha
Hawakuendelea kukaa macho na kusali
Kisha ufufuo wa Yesu, ni nini ilisaidia mitume wenye walitubu wasiangukie tena katika mutego wa kuogopa mwanadamu na waendelee kuhubiri hata kama kulikuwa upinzani?
Walikumbuka mashauri ya Yesu, na kwa hiyo, walikuwa tayari kupambana na mateso na upinzani
Walimutegemea Yehova na walisali.—Mdo. 4:24, 29
Ni hali gani zinaweza kutia ujasiri wetu katika jaribu?